Rocky Mountains (Kiing.
Mara nyingi hutazamiwa kuanza katika jimbo la British Columbia upande wa magharibi wa Kanada huelekea kusini hadi jimbo la New Mexico la Marekani. Urefu wa safu hii ni takriban kilomita 4,800. Mara nyingi hata milima ya Alaska na pia ya Meksiko ya kaskazini huhesabiwa kuwa sehemu za nje za Rockies.
Mlima mrefu ni Mount Elbert katika jimbo la Colorado mwenye kimo cha mita 4,401 juu ya UB. Mlima mkubwa katika Kanada ni Mount Robson wa British Columbia mwenye kimo cha mita 3,954.
Kijiolojia Rockies zimejitokeza kutokana kwa kugongana kwa mabamba ya gandunia yaani bamba la Pasifiki na bamba la Amerika ya Kaskazini. Mshtuko wa kugongana au kusukumana kwa mabamba haya yamekunja uso wa ardhi na kuzaa safu hii ya milima.
Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Rocky Mountains kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Rocky Mountains, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.