Fly540: Ni kampuni ya ndege inayosafirisha kwa gharama nafuu mjini Nairobi

Fly540 (kwa Kiingereza: Five Forty Aviation Ltd.) ni kampuni ya ndege inayosafirisha kwa gharama nafuu mjini Nairobi, Kenya.

Husafirisha abiria na mizigo, nchini na pia kitaifa.

Fly540
Faili:Optimized image b9d4dbdd.png
IATA
5H
ICAO
FFV
Callsign
SWIFT TANGO
Kimeanzishwa 2006
Vituo vikuu Jomo Kenyatta International Airport
Ndege zake 5
Shabaha 14
Nembo Simplifly
Makao makuu Nairobi, Kenya
Watu wakuu Neil Steffen, Don Smith (Chief Exectutive Officer)
Tovuti http://www.fly540.com/

Historia

Kampuni hii ya usafiri wa ndege ilianza shughuli kati ya Nairobi na Mombasa tarehe 24 Novemba 2006. Awali ilisafiri mara mbili kwa siku kwa kutumia ndege ya ATR 42 yenye viti 48. Jina la kampuni linahusu bei yake ya nauli ambayo ni Sh 5,540 kwa watu wazima pamoja na nauli ya kurudi, kusafiri kati ya miji iliyotajwa hapo juu .

Lonrho Afrika ni mwekezaji mkubwa katika kampuni, ambapo ililipa dola milioni 1.5 ili kumiliki asilimia 49 za hisa.

Mwezi Mei mwaka wa 2007 kampuni ilileta ndege mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q100 ili kuongeza idadi ya wasafiri, na kuiruhusu kuendeleza njia mpya za usafiri wa ndani. Idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 93 hadi 171,160 mwaka uliOmalizika 30 Septemba 2008, kutoka 88,571 mwaka wa 2007. Wakati huohuo, kipengele cha mzigo kilifikia asilimia 63, kutoka asilimia 65,8 mwaka wa 2007.

Miradi ya Afrika

Fly540: Historia, Miradi ya Afrika, Shabaha 
Ndege aina ya ATR 42 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe

Mpango wa awali wa usafiri wa ndege ulikuwa - isipokuwa usafiri wa mizigo - mpango wa usafiri wa abiria kati ya Nairobi na Mombasa, na Kisumu ikawa shabaha mnamo Januari mwaka wa 2007. Usafiri wa kila siku kati ya Nairobi na Malindi uliongezwa katika idadi ya huduma mwezi wa Februari mwaka wa 2007.

Oparesheni za kimataifa Zilianzia katika Oktoba mwaka wa 2007 kwa kusafiri kati ya Juba katika Sudan Kusini na Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo . Entebbe iliongezwa katika Februari mwaka wa 2008. Kiwanda cha Nairobi kina mipango ya kuendelea upanuzi hadi Rwanda, Msumbiji na Burundi mwaka 2009 Lengo la Kampuni ni kuwa msafiri wa Afrika, kupitia upanuzi na nyongeza mbili za viwanda:

"... Tutafungua kituo Kigali na kisha twende Afrika Magharibi. Ghana itakuwa kiwanda cha Afrika Magharibi. Katika Kusini mwa Afrika, tutakuwa na kiwanda Angola, hivyo itakuwa kampuni ya usafiri wa ndege Afrika kwa gharama nafuu

Ilipokea ruhusa kuanza oparesheni nchini Angola mwezi Aprili 2009. Mipango ya kwanza ni usafiri wa ndani hadi Cabinda, Luanda, Soyo, Benguela, Huambo na Malanje lakini katika kanda upanuzi utafanyika haraka kama soko la ndani litaonyesha mafanikio yake Mwezi Juni 2009, iliripotiwa kuwa Fly540 ilikuwa ikitayarisha kuanzisha kiwanda nchini Zimbabwe

Shabaha

Kufikia Juni 2009, Fly540 ilikuwa na shabaha zifuatazo:

  • Kenya
    • Eldoret (Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Eldoret)
    • Kisumu (Uwanja Wa Ndege wa Kisumu)
    • Kitale (Uwanja Wa Ndege wa Kitale )
    • Lamu (Uwanja Wa Ndege wa Manda)
    • Lodwar (Uwanja Wa Ndege wa Lodwar)
    • Malindi (Uwanja Wa Ndege wa Malindi)
    • Masai Mara (Uwanja Wa Ndege wa Mara Serena )
    • Mombasa (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Moi)
    • Nairobi (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta)
  • Sudan
    • Juba (Uwanja Wa Ndege wa Juba)
    • Rumbek (Uwanja Wa Ndege wa Rumbek)
  • Tanzania
    • Kilimanjaro (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
    • Zanzibar (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar)
  • Uganda
    • Entebbe (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe)

Ndege

Fly540 ina ndege zifuatazo (kufikia Januari 2009):

  • 3 × ATR 42-320
  • 1 × Bombardier Dash 8-102
  • 2 × Embraer ERJ 135 LR

Katika Januari 2008, kampuni hii ilitia saini dola million 150 za Amerika kwa mkataba wa ATR nane hadi 72-500skupokezwa mwaka wa 2008 na 2009..

Ajali na matukio

Tarehe 13 Agosti 2008, ndege aina ya Fokker F27-500 ilipania karibu na Uwanja wa Ndege wa Namber Konton Mogadishu, Somalia. Wafanyikazi wa ndege wote watatu walikufa. Ndege ilisemekana ilikuwa ikisafirisha miraa. Ndege kuondoka kutoka Uwanja Wa Ndegewa Wilson mjini Nairobi. Nambari yake ya usajili ni 5Y BVF

Viungo vya nje

Marejeo

Tags:

Fly540 HistoriaFly540 Miradi ya AfrikaFly540 ShabahaFly540 NdegeFly540 Ajali na matukioFly540 Viungo vya njeFly540 MarejeoFly540KenyaKiingerezaNairobi

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

MariooUlumbiMbeyaAla ya muzikiVita Kuu ya Pili ya DuniaRupie ya Afrika ya Mashariki ya KijerumaniUchaguziUpinde wa mvuaKiunguliaMkoa wa MaraWizara za Serikali ya TanzaniaFasihi simuliziKoloniMalengo ya Kiswahili kuwa lugha ya taifaMwaniChristopher MtikilaAfrika ya Mashariki ya KijerumaniJoyce Lazaro NdalichakoMnyoo-matumbo MkubwaRaiaDiglosiaHaki za watotoWashambaaMazingiraWapareRufiji (mto)RitifaaMatiniJeshi la Ulinzi la Wananchi wa TanzaniaKata za Mkoa wa Dar es SalaamHistoriaUgandaMtandao wa kijamiiMwakaMuundo wa inshaAgano JipyaUnyenyekevuNyangumiSheriaBendera ya KenyaMarie AntoinetteKarafuuKata za Mkoa wa MorogoroTungo kishaziChristina ShushoManispaaMfuko wa Mawasiliano kwa WoteHistoria ya IranTanganyika African National UnionRicardo KakaHekaya za AbunuwasiMnyamaNguruweAmina ChifupaTanzaniaViwakilishiLilithJava (lugha ya programu)Utumbo mpanaHistoria ya UislamuSaratani ya mlango wa kizaziNomino za kawaidaUchumiKamusi za KiswahiliAunt EzekielDodoma (mji)KamusiUsafi wa mazingiraSiafuLady Jay DeeSaidi Salim BakhresaKitenzi kikuuMuundoHistoria ya Kiswahili🡆 More