Fly540 (kwa Kiingereza: Five Forty Aviation Ltd.) ni kampuni ya ndege inayosafirisha kwa gharama nafuu mjini Nairobi, Kenya.
Husafirisha abiria na mizigo, nchini na pia kitaifa.
Faili:Optimized image b9d4dbdd.png | ||||
| ||||
Kimeanzishwa | 2006 | |||
---|---|---|---|---|
Vituo vikuu | Jomo Kenyatta International Airport | |||
Ndege zake | 5 | |||
Shabaha | 14 | |||
Nembo | Simplifly | |||
Makao makuu | Nairobi, Kenya | |||
Watu wakuu | Neil Steffen, Don Smith (Chief Exectutive Officer) | |||
Tovuti | http://www.fly540.com/ |
Kampuni hii ya usafiri wa ndege ilianza shughuli kati ya Nairobi na Mombasa tarehe 24 Novemba 2006. Awali ilisafiri mara mbili kwa siku kwa kutumia ndege ya ATR 42 yenye viti 48. Jina la kampuni linahusu bei yake ya nauli ambayo ni Sh 5,540 kwa watu wazima pamoja na nauli ya kurudi, kusafiri kati ya miji iliyotajwa hapo juu .
Lonrho Afrika ni mwekezaji mkubwa katika kampuni, ambapo ililipa dola milioni 1.5 ili kumiliki asilimia 49 za hisa.
Mwezi Mei mwaka wa 2007 kampuni ilileta ndege mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q100 ili kuongeza idadi ya wasafiri, na kuiruhusu kuendeleza njia mpya za usafiri wa ndani. Idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 93 hadi 171,160 mwaka uliOmalizika 30 Septemba 2008, kutoka 88,571 mwaka wa 2007. Wakati huohuo, kipengele cha mzigo kilifikia asilimia 63, kutoka asilimia 65,8 mwaka wa 2007.
Mpango wa awali wa usafiri wa ndege ulikuwa - isipokuwa usafiri wa mizigo - mpango wa usafiri wa abiria kati ya Nairobi na Mombasa, na Kisumu ikawa shabaha mnamo Januari mwaka wa 2007. Usafiri wa kila siku kati ya Nairobi na Malindi uliongezwa katika idadi ya huduma mwezi wa Februari mwaka wa 2007.
Oparesheni za kimataifa Zilianzia katika Oktoba mwaka wa 2007 kwa kusafiri kati ya Juba katika Sudan Kusini na Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo . Entebbe iliongezwa katika Februari mwaka wa 2008. Kiwanda cha Nairobi kina mipango ya kuendelea upanuzi hadi Rwanda, Msumbiji na Burundi mwaka 2009 Lengo la Kampuni ni kuwa msafiri wa Afrika, kupitia upanuzi na nyongeza mbili za viwanda:
"... Tutafungua kituo Kigali na kisha twende Afrika Magharibi. Ghana itakuwa kiwanda cha Afrika Magharibi. Katika Kusini mwa Afrika, tutakuwa na kiwanda Angola, hivyo itakuwa kampuni ya usafiri wa ndege Afrika kwa gharama nafuu
Ilipokea ruhusa kuanza oparesheni nchini Angola mwezi Aprili 2009. Mipango ya kwanza ni usafiri wa ndani hadi Cabinda, Luanda, Soyo, Benguela, Huambo na Malanje lakini katika kanda upanuzi utafanyika haraka kama soko la ndani litaonyesha mafanikio yake Mwezi Juni 2009, iliripotiwa kuwa Fly540 ilikuwa ikitayarisha kuanzisha kiwanda nchini Zimbabwe
Kufikia Juni 2009, Fly540 ilikuwa na shabaha zifuatazo:
Fly540 ina ndege zifuatazo (kufikia Januari 2009):
Katika Januari 2008, kampuni hii ilitia saini dola million 150 za Amerika kwa mkataba wa ATR nane hadi 72-500skupokezwa mwaka wa 2008 na 2009..
Tarehe 13 Agosti 2008, ndege aina ya Fokker F27-500 ilipania karibu na Uwanja wa Ndege wa Namber Konton Mogadishu, Somalia. Wafanyikazi wa ndege wote watatu walikufa. Ndege ilisemekana ilikuwa ikisafirisha miraa. Ndege kuondoka kutoka Uwanja Wa Ndegewa Wilson mjini Nairobi. Nambari yake ya usajili ni 5Y BVF
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Fly540, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.