Manuel Ellis alikuwa mtu Mweusi mwenye umri wa miaka 33 ambaye alifariki mnamo Machi 3, 2020, wakati alipokamatwa na maafisa wa polisi huko Tacoma, Washington.
Makala hii au sehemu ya makala hii inahitaji masahihisho kwa upande mmoja wa zifuatazo: Ili kupata sababu angalia ukurasa wa majadiliano. |
Idara ya sherifu ya jimbo la Pierce hapo awali ilidai kuwa Ellis alishambulia gari la polisi na kisha kuwashambulia maafisa, na kupelekea kukamatwa. Waendesha mashtaka wa serikali waliwanukuu mashahidi wa kiraia wakisema kwamba Ellis hakushambulia gari la polisi au maafisa; walisema pia ni maafisa ndio walioanzisha matumizi ya nguvu kwa Ellis baada ya mazungumzo. Video ya tukio hilo ilionyesha maafisa wakimpiga Ellis mara kwa mara, kumkaba, kwa kutumia kiwiko, na kumpigisha magoti. Waendesha mashtaka wa serikali walisema kwamba "Ellis hakuwa akipigana", wakitoa maelezo ya mashahidi na ushahidi wa video. Rekodi ya redio ya polisi ilionyesha kuwa Ellis alisema "hawezi kupumua".
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uuaji wa Manuel Ellis, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.