Filipo II wa Masedonia (kwa Kigiriki: Φίλιππος Β΄ ὁ Μακεδών, Phílippos II ho Makedṓn; 382 KK – 336 KK) alikuwa mfalme wa Masedonia katika Ugiriki wa Kale kuanzia mwaka 359 KK hadi alipouawa.
Mnamo 500 KK kulikuwako ufalme ulioitwa Masedonia ambao ulihesabiwa kama sehemu ya utamaduni wa Ugiriki wa kale na wafalme waliruhusiwa kwenye michezo ya Olimpiki ya madola ya Wagiriki.
Pamoja na sehemu nyingi za Ugiriki ufalme huo ulipaswa kukubali ubwana wa Milki ya Uajemi, lakini Filipo alifaulu kuurudisha uhuru akaendelea kuifanya Masedonia kuwa dola kiongozi kati ya madola madogo ya Ugiriki.
Mwanawe Aleksanda Mkuu aliimarisha utawala wake juu ya Wagiriki wengine na kushambulia Milki ya Uajemi na hatimaye kuivamia na kuishinda kwa jeshi kutoka sehemu zote za Ugiriki.
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Filipo II wa Masedonia kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Filipo II wa Masedonia, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.