Kilifi ni mji kwenye pwani ya Kenya uliopo kati ya Mombasa na Malindi.
Iko kando ya kihori cha Kilifi ("Kilifi Creek") kinachoishia katika Bahari Hindi.
Kilifi | |
Mahali pa mji wa Kilifi katika Kenya | |
Majiranukta: 3°38′0″S 39°51′0″E / 3.63333°S 39.85000°E | |
Nchi | Kenya |
---|---|
Kaunti | Kilifi |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 122,899 |
Mji ni makao makuu ya Kaunti ya Kilifi.
Wakati wa sensa ya mwaka 2009 Kilifi ilikuwa na wakazi 122,899 .
Kilifi imekuwa kitovu kimojawapo cha utalii nchini Kenya hasa kutokana na fuko zake za kupendeza na Bofa Beach ni marufuku hasa. Mdomo mpana wa kihori unapendwa na wenye jahazi za burudani kuna jahazi nyingi zinazolala hapa.
Maghofu ya kihistoria ya Mnarani yako kando la mji wa Kilifi. Mabaki yanayoonekana ni misikiti mbili pamoja na makaburi yaliyokuwa sehemu ya mji wa Waswahili uliokuwa kituo cha biashara. Msikiti mkubwa ulianzishwa mnamo mwaka 1425; mji uliangamizwa wakati wa mashambulio ya Waoromo katika karne ya 17.
Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kilifi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kilifi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.