Wakatoliki wa Kale ni jina linalotumika kujumlisha Wakristo wa Magharibi ambao wametengana na Askofu wa Roma hasa baada ya Mtaguso wa kwanza wa Vatikano (1869-1870) kutangaza dogma ya Papa kutoweza kukosea anapotamka rasmi jambo fulani kama fundisho la kudumu moja kwa moja.
Wakristo hao walijipatia uaskofu halisi katika mlolongo wa Mitume kupitia Askofu wa Utrecht mwaka 1873, na baada ya hapo waliusambaza kwa madhehebu mengi, ambayo mengine kwa sasa hayana ushirika nao.
Kumbe Wakatoliki wa Kale wana ushirika na Waanglikana.
Imani na liturujia zao zinafanana na zile za Kanisa Katoliki, lakini taratibu zimekwenda mbali, kwa mfano kwa kukubali upadri kwa wanawake na kwa kiasi fulani ushoga.
Baadhi ya Makanisa ya namna hiyo yanaunda "Umoja wa Utrecht" ulioanzishwa mwaka 1889 na kuwa na waamini 115,000 duniani mwaka 2016, wakiwa karibu wote wakazi wa Ulaya Magharibi na Poland.
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wakatoliki wa Kale kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Wakatoliki wa Kale, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.