Uzoroasta ni dini na falsafa inayopata jina lake kutoka nabii wake Zoroasta au Zarathustra, ambayo iliathiri imani ya Uyahudi na ya dini zilizotokana na Uyahudi.
Wazoroasta wanaamini katika ulimwengu na Mungu apitaye fikira, Ahura Mazda, ambaye ibada zote zinaelekezwa kwake.
Kiumbe cha Ahura Mazda ni asha, ukweli na mpango, ambaye anazozana na kinyume chake, druj, uongo na machafuko.
Kwa sababu binadamu ana hiari, watu lazima wawe na uwajibikaji kwa maadili wanayoyachagua. Kwa kutumia hiari, watu lazima wawe na jukumu tendaji katika mgogoro wa dunia nzima, na mawazo mema, maneno mema na matendo mema ili kuhakikisha furaha na kuepuka machafuko.
Zamani dini iliyo ilikuwa kubwa, lakini siku hizi imebaki na wafuasi 127,000 hadi 190,000 tu. Jumuiya ya takriban Wazoroasta 25,000 wanaishi katika nchi ya asili yao Uajemi (Iran), hasa katika mazingira ya Kerman na Yazd, na pia katika miji mikubwa kama Tehran. Jumuiya kubwa nyingine yenye watu 57,264 inapatikana Uhindi wanapojulikana kwa jina la Waparsi ("Parsee"); wametokana na Wazoroasta kutoka Uajemi waliokimbilia Uhindi wakati jumuiya yao ilipoteswa katika nchi ya asili.
Kutoka Uajemi na Uhindi walihamia mara nyingi kwa hiyo leo hii kuna jamii zao pia Marekani, Kanada na Ulaya. Idadi yao inapungua polepole kwa sababu ni wagumu sana kupokea waumini wapya kutoka dini nyingine ilhali hawakubali tena watoto wao kuwa Wazoroasta wakifunga ndoa nje ya jumuiya.
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uzoroasta, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.