Umaskini: Ukosefu wa kiasi fulani cha mali au fedha

Umaskini (kutoka neno la Kiarabu) ni hali ya ukosefu wa mahitaji ya msingi ya binadamu kama vile chakula, maji salama, huduma za afya, mavazi na nyumba kutokana na kukosa uwezo wa kuvinunua.

Hii pia inajulikana kama umaskini uliokithiri au ufukara.

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini
Mtaa wa mabanda mjini Jakarta, Indonesia

Umaskini wa kadiri ni kuwa na rasilmali chache zaidi au mapato madogo zaidi kulingana na watu wengine katika jamii au nchi au hali ya wastani duniani. Hali hii pia hujulikana kama umaskini halisi au unyonge. Umaskini linganishi ni hali ya kuwa na rasilimali chache au kipato cha chini kuliko wengine kwenye jamii au nchi, au ikilinganishwa na wastani duniani kote.

Umaskini unajumlisha pia matokeo yake upande wa siasa na jamii.

Kupunguza ufukara ni kati ya malengo makuu ya taasisi nyingi za kimataifa, kama vile Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia. Benki hiyo imekadiria kuwa watu milioni 702.1 walikuwa wakiishi kifukara mno mwaka 2015, wakati walikuwa bilioni 1.75 mwaka 1990 (kutoka 37.1% hadi 9.6%).

Kati yao, milioni 347.1 hivi walikuwa Afrika Kusini kwa Sahara (35.2% za wakazi) na 231.3 Asia Kusini (13.5%), lakini ufukara ni changamoto kwa nchi zote duniani.

UNICEF imekadiria kwamba nusu ya watoto wote duniani wanaishi kifukara (bilioni 1.1).

Wataalamu mbalimbali wamesema sera za uliberali mpya zinazofuatwa na taasisi za kiuchumi za kimataifa (kama vile IMF na Benki ya Dunia) zinazidisha tofauti za kiuchumi kati ya binadamu.

Asili ya umaskini

Asili ya umaskini inahusika hasa na sababu za kiwango cha chini cha utajiri na uzalishaji cha watu maskini au, ikisemwa vingine, uhaba na mfumuko wa bei wa bidhaa ambazo wanazitumia.

Vikwazo kwa uzalishaji

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Watoto wasio na makao wakilala katika Mtaa wa Mulberry-Picha ya Jacob Riis, New York, Marekani (1890).
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Watu wasio na makao wanaishi katika nyumba zilizojengwa kwa makaratasi mjini Los Angeles, California.

Ukosefu wa nia ya serikali na ya watu wa tabaka la juu ya kuwapa wapangaji wao haki kamili ya kumiliki ardhi imetajwa kama kikwazo kikuu kwa maendeleo.

Utovu wa uhuru wa kiuchumi ni kizingiti kikubwa kwa ujasiriamali wa watu maskini.

Biashara mpya na wawekezaji kutoka nchi za nje wanaweza kufukuzwa kutokana na kuwepo kwa taasisi zinazoongozwa vibaya, hasa kutokana na ufisadi, udhaifu wa sheria na vikwazo vingi vya urasimu. Nchini Kanada, itamchukua mfanyabiashara siku mbili, hatua mbili za kiurasimu na dola 280 kufungua biashara ilhali mfanyabiashara nchini Bolivia analazimishwa kulipa dola 2,696 kama ada, angojee siku 82 za kazi, na apitie hatua 20 ili kufanya jambo lilelile.

Vikwazo vikuu kama hivi hufaidi zaidi biashara kubwa na kuzidhoofisha biashara ndogo, ambako idadi kubwa ya nafasi za kazi huundwa nchini India kabla ya mabadiliko ya kiuchumi, wenye biashara walipaswa kuwahonga wafanyakazi wa serikali ili wafanye kazi zao za kila siku, na ilikuwa kama ushuru kwenye biashara yao.

Ufisadi nchini Nigeria, kwa mfano mapato yanayotokana na uuzaji wa mafuta yanayokadiriwa kuwa dola bilioni 400 yameibwa na viongozi wa nchi kati ya miaka 1960 na 1999

Utovu wa nafasi pia unaweza kusababishwa na serikali kutojenga miundombinu bora.

Nafasi bora za kazi katika mataifa tajiri zaidi husababisha watu wenye vipawa maalum kuhama, na hivyo kuwapoteza wataalamu. Kupotea huku kunaligharimu bara la Afrika zaidi ya Dola bilioni 4 zinazotumika kuajiri zaidi ya wataalamu 150,000 kutoka nchi za ng’ambo kila mwaka.

Wanafunzi wa India wanaokwenda ng’ambo kuendelea na masomo yao huigharimu nchi yao mapato yanayotokana na fedha za kigeni yanayofika Dola bilioni 10 kila mwaka

Afya duni na ukosefu wa elimu nafuu huathiri vibaya uzalishaji. Ukosefu wa chakula cha kutosha utotoni huathiri uwezo wa mtu kukua na kutumia vipawa vyake. Ukosefu wa madini muhimu kama vile iodini na chuma unaweza kuzuia kukua kwa ubongo. Watu bilioni mbili (theluthi moja ya watu wote duniani) wameathiriwa na ukosefu wa iodini mwilini. Katika mataifa yanayoendelea, inakadiriwa kuwa asilimia 40 ya watoto wenye umri wa miaka minne kwenda chini wana ugonjwa wa anemia kutokana na ukosefu wa madini ya chuma katika chakula chao.

Vilevile matumizi mabaya ya dawa, ulevi wa pombe na madawa ya kulevya vinaweza kuwaweka watu katika hali ya umaskini unaoendelea.

Maradhi ya kuambukiza kama vile malaria na kifua kikuu yanaweza kusababisha umaskini kwani maradhi haya hutumia raslimali zote za kifedha na afya ambazo zingetumiwa katika uwekezaji na uzalishaji. Malaria hupunguza ukuaji wa pato la kitaifa kwa asilimia 1.3 katika baadhi ya mataifa yanayoendelea ilhali Ukimwi hupunguza ukuaji wa Afrika kwa kati ya asilimia 0.3 na 1.5 kila mwaka.

Vita, migogoro ya kisiasa na uhalifu, vinavyojumuisha vikundi haramu vinavyozua vurugu na vikundi vya walanguzi wa madawa ya kulevya pia vinaweka vikwazo kwa uwekezaji. Vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro barani Afrika pia vimeligharimu bara hilo dola bilioni 300 kati ya miaka 1990 na 2005. Eritrea na Ethiopia zilitumia mamilioni ya madola katika vita vilivyosababisha mabadiliko madogo ya mipaka yao.

Kutokana na hali ya mzunguko wa biashara kiwango cha umaskini kinaweza kuongezeka wakati uchumi unapozorota na kushuka kiwango cha umaskini kinaweza kuongezeka wakati wakati uchumi unapofanya vizuri. Vipengele vya utamaduni, kama vile ubaguzi wa aina mbalimbali, unaweza kuathiri vibaya uzalishaji kama vile ubaguzi kwa msingi wa umri , sifa mbaya, ubaguzi wa kijinsia, ubaguzi wa rangi na ubaguzi wa kitabaka.

Max Weber aliandika ya kuwa maadili ya kiutamaduni yanaweza kuathiri maafikiano ya kiuchumi.

Hata hivyo, watafiti wengine wamekusanya ushahidi unaoonyesha kuwa maadili hayajakita mizizi inavyodhaniwa na kuwa kubadilika kwa nafasi za kiuchumi hueleza zaidi msongamano ndani na nje ya umaskini kinyume na mabadiliko ya maadili.

Upungufu wa mahitaji ya msingi

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Meza za upasuaji zilizotengenezwa kwa mbao ngumu ni za kawaida katika kliniki zilizo katika maeneo ya mashambani ya Nigeria.

Kupanda kwa gharama ya maisha kunawafanya maskini wawe maskini zaidi. Kiwango kikubwa cha bajeti za watu maskini hutumika kununua chakula ikilinganishwa na matajiri. Kutokana na jambo hili, jamii za watu maskini na wale wanaokaribia umaskini huathiriwa kwa kiasi kikubwa na ongezeko la bei ya vyakula. Kwa mfano, mwishoni mwa mwaka 2007 kupanda kwa bei ya nafaka kulizua rabsha katika mataifa kadhaa. Benki ya Dunia ilionya ya kuwa watu milioni 100 walikuwa na hatari ya kuwa maskini zaidi.

Ukame na uhaba wa maji pia vinaweza kuwa tishio kwa usambazaji wa chakula.

Kulima mashamba mfululizo, majira baada ya majira, humaliza rutuba ya udongo na mwishowe hupunguza mazao ya kilimo. Inakadiriwa ya kuwa asilimia 40 ya mashamba duniani yameharibika vibaya. Barani Afrika, ikiwa mwendo huu wa kuharibika kwa udongo utaendelea, bara hilo litaweza kulisha asilimia 25 tu ya watu wanaoishi humo kufikia mwaka 2025.

Watu maskini hawapati huduma za afya kwa urahisi. Uhamaji kutoka nchi maskini wa wafanyakazi wanaotoa huduma hizo umeathiri vibaya nchi hizo. Kwa mfano, wauguzi 100,000 kutoka Ufilipino walihama kati ya miaka 1994 na 2006. Kuna madaktari Waethiopia wengi zaidi mjini Chicago kuliko wale walioko Uhabeshi.

Ongezeko la idadi ya watu na ukosefu wa huduma za uzazi wa mpango vinatajwa pengine kati ya sababu za umaskini: hata hivyo ni vyema kutambua ya kuwa watu huongezeka taratibu tu au hata idadi yao inaweza kupungua. Hii inatokana na mabadiliko kama vile kiwango cha vifo na kiwango cha waliozaliwa na jinsi zinavyoathiri idadi ya watu

Athari za umaskini

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Tena katika nchi iliyoendelea watu wameziacha nyumba za baraza huko Seacroft, Leeds, Uingereza kutokana na kuongezeka kwa umaskini na uhalifu .

Athari za umaskini pia zinaweza kuwa vyanzo, kama ilivyoorodheshwa hapo juu, na hivyo kuunda “mzunguko wa umaskini” unaodhihirika katika ngazi mbalimbali: ya kibinafsi, ya kimtaa, kitaifa na kimataifa.

Afya

    Makala kuu: Maradhi ya ufukara

Theluthi moja ya vifo - watu milioni 18 hivi kwa mwaka au watu 50,000 kwa siku - vinatokana na sababu zinazohusiana na umaskini. Kwa jumla, watu milioni 270, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wamefariki kutokana na umaskini tangu 1990. Wale ambao wanaishi katika umaskini wanateseka kwa viwango visivyo sawa kutokana na njaa au hata ukosefu wa chakula na magonjwa.

Wale wanaoishi kwa umaskini huishi miaka michache zaidi. Kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO), njaa na ukosefu wa lishe bora ndilo tishio kuu zaidi kwa afya ya umma duniani na ukosefu wa lishe bora ndio unaochangia pakubwa vifo vya watoto, katika nusu ya kesi zote. Kila mwaka karibu watoto milioni 11 wanaoishi katika umaskini hufa kabla ya kufikisha miaka mitano. Watu bilioni 1.02 hulala bila chakula kila siku.

Umaskini huongeza hatari ya ukosefu wa makazi. Kuna zaidi ya watoto wasio na makao milioni 100 duniani.

Ongezeko la tishio la matumizi ya madawa ya kulevya pia linaweza kuhusishwa na umaskini. Kulingana na Kipimo cha Kiwango Cha Njaa Duniani, Asia ya Kusini ina kiwango kikubwa zaidi duniani cha watoto wanaokosa lishe bora. Karibu nusu ya watoto wote nchini Uhindi hawapati chakula cha kutosha, mojawapo wa viwango vikubwa zaidi duniani na ni karibu mara mbili ya kiwango cha Kusini kwa Sahara barani Afrika.

Kila mwaka, zaidi ya wanawake nusu milioni wanakufa kutokana na mimba au wakati wa kujifungua. Karibu asilimia tisini za vifo vya wakina mama hutokea katika Asia na kusini kwa Sahara barani Afrika, ikilinganishwa na chini ya asilimia moja katika nchi zilizoendelea duniani.

Elimu

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Wakati uchumi wa dunia ulipofifia kabisa: mwanaume amelala chini kwenye gati, katika gudi za jiji la New York, 1935.

Uchunguzi umedhihirisha ya kuwa watoto wanaotoka katika jamii zenye mapato ya chini wanakumbana na tishio kubwa la kutofanya vyema katika masomo yao. Mara nyingi, jambo hili huanza kuwadhuru watoto hawa wakiwa wangali katika kiwango cha shule ya msingi. Katika mfumo wa elimu wa Amerika, watoto hao hupata tishio kubwa zaidi, ikilinganishwa na watoto wengine, ya kutopata gredi nzuri shuleni, kuwekwa katika maeneo maalum yaliyotengwa wakati wa masomo shuleni na hata kukosa kumaliza masomo yao ya shule ya upili. Kuna mambo kadhaa yanayoeleza sababu za wanafunzi kuwa na mazoea ya kuacha shule. Kwa watoto walio na rasilimali kidogo, tishio linatokana na sababu kama vile viwango vya watoto waliovunja sheria, viwango vya juu vya watoto waliopata mimba, wakiwa wachanga na kutegemea kiuchumi mzazi au wazazi wenye mapato ya chini.

Familia na jamii zisizotilia maanani uwekezaji katika elimu na maendeleo ya watoto maskini hupata matokeo yasiyo mazuri kwani baadaye watoto hawa hukosa kazi na huwa na mapato madogo. Viwango vikubwa zaidi vya kuzaa mapema na hatari zake kwa familia, afya na maisha bora kwa ujumla ndiyo mambo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa kwa kuwa elimu kutoka kiwango cha shule ya chekechea hadi shule ya upili ina umuhimu mkuu maishani.

Umaskini mara nyingi huathiri, kwa kiwango kikubwa, kufaulu kwa watoto shuleni. “Shughuli za mtoto akiwa nyumbani, yale anayoyapendelea, upekee wake” vyote vinapaswa kulingana na hali ilivyo duniani kwani ikiwa havilingani, wanafunzi hao hawatafaidika wakiwa shuleni na hasa darasani. Kwa hiyo, tunaweza kusema kuwa watoto wanaoishi katika hali ya umaskini au chini ya kiwango cha umaskini watakuwa na wakati mgumu zaidi kufaulu katika elimu kuliko watoto wanaoishi katika hali isiyo ya umaskini. Watoto maskini hawapati huduma muhimu za afya na hii inawafanya wakose kwenda shuleni kwa siku nyingi katika mwaka. Pia, kuna uwezekano zaidi kwa watoto maskini kuteseka kwa njaa, uchovu, kukasirika ovyo, maumivu ya kichwa, maambukizi ya masikio, mafua na homa. Magonjwa haya yana uwezo wa kumzuia mtoto au mwanafunzi kuelewa yale anayofunzwa darasani.

Ukatili

Maeneo yaliyoathiriwa sana na umaskini mara nyingi huwa na ukatili mwingi. Katika uchunguzi mmoja, asilimia 67 ya watoto kutoka jamii maskini katika maeneo yenye makazi duni walisema ya kuwa walishuhudia mashambulio makali, na asilimia 33 wakaripoti kushuhudia mauaji. Asilimia 51 ya wanafunzi wa darasa la tano mjini New Orleans (kiwango cha wastani cha mapato kwa kila jamii: Dola 27,133 za Amerika) wameathiriwa wa ukatili, ikilinganishwa na asilimia 32 huko Washington, DC (kiwango cha wastani cha mapato kwa kila jamii: Dola 40,127 za Amerika).

Madhara ya muda mrefu

Baadhi ya madhara marefu ya umaskini huathiri watoto kabla hata kuzaliwa. Wanawake walio na watoto waliozaliwa katika umaskini, hawawezi kulisha watoto kwa ufanisi na kwa malezi ya haki. Wanaweza pia kuugua ugonjwa ambazo zinaweza kuambukizwa kwa mtoto kwa kupitia kuzaliwa. Pumu ni tatizo la kawaida kwa watoto kupata wakati wanapozaliwa katika umaskini. Chakula a msaada hasa hutumiwa na watu ambao wanaishi katika kipato cha chini. Talaka, kifo, ulevi, na kupoteza kazi ni chache tu kati ya hali zinazoweza kutokana na umaskini. Wanafunzi katika darasa azilishi za shule wanaoishi katika umaskini wanalazimishwa sana kuondoka na kuzunguka kuhudhuria shule za asili zinazofadhiliwa. Hawa wanafunzi hupambana katika shule. Elimu ya umaskini humweka mtoto katika hali ya kupambana baadaye. Vijana ambao wanaishi katika umaskini ni wanaelekea zaidi kuhusika na madawa ya kulevya, pombe, kinyume cha vitendo, na kundi shughuli.

Kupunguza umaskini

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Idadi ya watu duniani wanaoishi katika hali ya umaskini uliokithiri imepungua kwa asilimia 50 tangu 1981. Jedwali lnaonyesha makisio na makadirio kutoka Benki ya Dunia kati ya 1981 na 2009.
    Makala kuu: Kupunguza ufukara

Kulingana na historia, kupunguka kwa umaskini kumetokana kwa kiasi kikubwa na ukuaji wa uchumi kwa ujumla. Umaskini ulikuwa umekubalika na wengi kama jambo lisiloweza kuepukika na nchi zilizalisha kwa kiwango kidogo sana kabla ya mapinduzi ya viwanda, ambayo yalisababisha ukuaji wa kiuchumi kwa kiasi kikubwa. Jambo hili liliwaokoa wengi na umaskini katika mataifa ambayo kwa sasa yanajulikana kama mataifa yaliyoendelea Katika mwaka 1820, asilimia 75 ya wanadamu waliishi kwa chini ya dola moja kwa siku, na kufikia mwaka wa 2001 ni asilimia 20 pekee walioishi kwa dola moja kwa siku. Ukuaji wa uchumi unaotokana na ukulima, kwa wastani, umefaulisha mara mbili zaidi nusu ya walio maskini sana katika nchi ikilinganishwa na ukuaji unaotokana na sekta zingine zisizo za ukulima. Hata hivyo, msaada ili kuhakikisha ya kuwa wale ambao tayari ni maskini watapata maisha bora zaidi na pia kuifadhili mikakati ya kimatibabu na kisayansi kama vile green revolution na kutokomeza ndui.

Uhuru wa kiuchumi

Mojawapo kati ya njia bora zaidi za kupunguza umaskini katika nchi yoyote ni kuhakikisha kuwa haki ya maskini ya kumiliki mali imelindwa. Ulindaji wa haki ya kumiliki ardhi, ambayo ni raslimali kubwa zaidi katika jamii nyingi, ni muhimu katika kuhakikisha uhuru wa kiuchumi. Benki ya Dunia inasema ya kuwa kuhakikisha haki ya kumiliki ardhi ndio “ufunguo wa kupunguza umaskini” ikiongeza kusema kuwa haki ya kumiliki ardhi inaongeza utajiri wa watu maskini, na wakati mwingine inaweza kuuongeza maradufu. Inakadiriwa ya kuwa ikiwa serikali zitatambua haki ya maskini ya kumiliki mali, jambo hili litawapa raslimali ambayo kwa ujumla ni mara 40 ya misaada yote ya kigeni tangu mwaka wa 1945. Ingawa mbinu zilizotumiwa ni tofauti, Benki kuu ya Dunia inasema ya kuwa maswala makuu ni yale ya haki ya umiliki na kuhakikisha ya kuwa ardhi inauzwa kwa bei nafuu.

Nchini Uchina na India kupunguka kwa umaskini kwa muda wa miongo michache iliyopita kumetokana na kuacha ukulima wa pamoja nchini Uchina na kuondolewa kwa urasimu mwingi serikalini nchini India. Hata hivyo, kukatizwa kwa ufadhili wa serikali katika miradi ya kijamii, ambayo pia inajulikana kama kanuni ya soko huru wakati mwingine huleta matokeo ya kusikitisha. Kwa mfano, Benki ya Dunia hushurutisha mataifa maskini kuondoa ruzuku kwa mbolea na ilhali wakulima wengi hawawezi kumudu bei hizi sokoni. Kubadilishwa kwa mfumo wa ugawaji wa fedha katika mataifa ya awali ya Urusi ya zamani wakati wa mpito kuelekea uchumi wa kibepari kulipendekeza kupunguza matumizi ya fedha katika sekta za afya na elimu na hivyo kuongeza umaskini kwa kiasi kikubwa.

Kuanzishwa kwa soko huria kunaongeza ujumla wa bidhaa za nchi zinazofanya biashara pesa zinazotumwa kuelekea nchi maskini kama vile India, wakati mwingine hushinda uwekezaji kutoka nchi za kigeni na ni zaidi ya mara mbili ya msaada kutoka kwa nchi wanachama wa OECD (Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo). Uwekezaji wa kigeni na viwanda vinavyotengeneza bidhaa zinazouzwa katika nchi za nje zimechangia kupanuka kwa uchumi wa nchi za Bara Asia zinazokua kwa kasi mno.

Hata hivyo, kanuni za biashara mara nyingi huwa si za haki kwa kuwa zinazuia nchi maskini kuingia katika masoko ya nchi tajiri na pia zinapiga marufuku nchi maskini kujiendeleza kiviwanda. Bidhaa zilizotengenezwa viwandani kutoka nchi maskini hutozwa ushuru zaidi ikilinganishwa na malighafi zinapowasili katika bandari za nchi tajiri. Uchunguzi uliofanywa na Chuo Kikuu cha Toronto ulionyesha ya kuwa kodi iliyotozwa maelfu ya bidhaa kutoka Afrika na taifa ilishuka baada ya kuundwa kwa mkataba wa AGOA uliochangia pakubwa kuwepo kwa “idadi kubwa ya kushangaza” ya bidhaa zinazoagizwa kutoka Afrika.

Mikataba pia inaweza kujadiliwa ili kuzipendelea zaidi nchi zinazoendelea kama vile ilivyofanywa nchini Thailand, ambako kanuni ya asilimia 51 inalazimisha kampuni za kimataifa zinazoanza kuendesha biashara nchini humo kutoa asilimia 51 ya udhibiti kwa kampuni zao kwa kampuni nyingine nchini Thailand, yaani ni lazima kampuni za kimataifa zishirikiane na kampuni za humo nchini.

Rasilmali, miundomsingi na teknolojia

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Pato la dunia kwa kila mtu

Uwekezaji katika mtaji wa binadamu kwa njia ya afya unahitajika ili kuhakikisha ukuaji wa uchumi. Si lazima mataifa yawe na utajiri ili yawe na afya. Kwa mfano, Sri Lanka ilikuwa na kiwango cha vifo vya mama wajawazito cha asilimia 2 katika miaka ya 1930 idadi kubwa zaidi ikilinganishwa na nchi yoyote kwa sasa. Kiwango hiki kilipunguka hadi kati ya asilimia 0.5 na asilimia 0.6 katika miaka ya 1950 na asilimia 0.06 hivi sasa Hata hivyo, Sri Lanka ilikuwa ikitumia pesa kidogo zaidi kwa afya ya uzazi kwa kuwa ilishajifunza njia mwafaka za kukabiliana na matatizo hayo.

Ingawa hakuna ufahamu kuhusu manufaa ya kifedha yanayotokana na kutoa huduma za afya, mikakati ya kuwaelimisha watu imewekwa kama vile mipango iliyopewa kipaumbele ya kudhibiti magonjwa. [5] Archived 6 Aprili 2006 at the Wayback Machine. Kuwaelimisha watu kuhusu umuhimu wa kuosha mikono ni moja kati ya mikakati ya afya isiyo na gharama na inaweza kupunguza vifo vinavyotokana na magonjwa yanayowaathiri watoto kama vile kuhara na nimonia kwa asilimia 50. Mtaji wa binadamu, kwa kupitia elimu, ni kipengee muhimu zaidi kinachoathiri ukuaji wa uchumi kushinda mtaji wa vitu vinavyoonekana na kushikika.

Wanauchumi wa Umoja wa Mataifa wanasema ya kuwa miundomsingi bora kama vile barabara na mtandao wa habari husaidia kufanikisha mabadiliko katika soko. Nchi ya Uchina inasema ya kuwa inafanya uwekezaji katika reli, mabarabara, bandari na simu katika maeneo ya mashambani barani Afrika kama sehemu ya mbinu zake za kuhakikisha maendeleo ya kiuchumi. Hapo awali, teknolojia ya mtambo unaotumia mvuke ndiyo iliyoanza kupunguza viwango vya umaskini. Teknolojia ya simu za mkononi inaleta soko kwa sehemu maskini au za mashambani. Kutokana na maarifa wanayoyapata, wakulima vijijini wanaweza kuzalisha mimea maalum ambayo watawauzia wanunuzi na kupata faida.

Teknolojia kama hiyo pia inazifanya huduma za kifedha ziweze kupatikana kwa urahisi kwa watu maskini. Kwa wale wanaoishi katika hali ya umaskini, inasisitizwa kwamba wawe na sehemu zenye usalama wa kutosha ili waweze kuweka akiba badala ya kungojea mikopo. Pia, kiwango kikubwa cha mikopo kwa wafanyibiashara wadogo kinatumika kwa bidhaa ambazo zinaweza kununuliwa kwa kutumia fedha zilizo katika akaunti za akiba. Huduma za benki kupitia simu za mkononi zimesaidia kutatua shida ya masharti mengi na ulipaji wa ada nyingi za kuendesha akaunti za akiba s. Huduma za fedha kupitia simu za mkononi katika nchi zinazoendelea, na ambazo zimezipita nchi zilizoendelea katika nyanja hizi, inakadiriwa kuwa Dola bilioni tano kufikia mwaka 2012. Kampuni ya Safaricom ilianzisha huduma inayojulikana kama M-Pesa mojawapo kati ya mfumo wa kwanza unaotumia mtandao wa maajenti, wengi wao wakiwa ni wenye duka, badala ya matawi ya benki kuchukua pesa taslimu zinazowekwa na kuziweka katika akaunti zilizoundwa katika simu za wateja hao. Shughuli za kutuma na kupokea pesa hufanywa kati ya simu za wanaohusika. Ada ndogo inatolewa, na hii inahakikisha usalama wa pesa zinazotumwa kutoka.

Msaada

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Wananchi kutoka kijiji cha Janabi wakingojea kukusanya bidhaa kutoka kwa Wana wa Iraq (Abna al-Iraq) katika oparesheni ya kijeshi iliyoandaliwa na kampuni ya kikundi kidogo cha tatu cha wanajeshi wa Charlie Company, kikundi kikubwa cha tatu cha 187 Infantry Regiment, Kitengo cha 101 cha Airbone, Yusufiah, Iraq, tarehe 2 Machi 2008. (Picha ya Jeshi la Amerika imepigwa na Spc Luke Thornberry)
    Makala kuu: Msaada, Ustawi wa jamii, Misaada ya maendeleo, na Kusamehe madeni

Msaada unaweza kufafanuliwa kama mapato ya kimsingi ya ruzuku,aina ya mpango wa kijamii ambapo wananchi hupewa pesa baada ya muda uliotengwa. Katika miradi ya majaribio nchini Namibia, ambako mradi kama huu hulipa Dola 13 pekee kila mwezi, watu waliweza kulipa karo ya shule na hivyo idadi ya watoto walioenda shuleni ikapanda kwa asilimia 92, kiwango cha ukosefu wa lishe bora kwa watoto kulishuka kutoka asilimia 42 hadi asilimia 10, na shughuli za kiuchumi zikapanda kwa asilimia 10.

Msaada pia ulitolewa ikiwa kanuni fulani zilifuatwa. Ugawaji wa fedha kwa kufuata kanuni maalum imesifiwa na wengi kama njia mwafaka ya kukabiliana na umaskini. Fedha hutolewa tu baada ya kufuata kanuni fulani kama vile kuwapeleka watoto shuleni au kuhakikisha wa kuwa watoto wamechanjwa. Nchini Mexico, kwa mfano, ambayo ni nchi iliyo na mradi mkubwa zaidi kama huu, idadi ya wanafunzi wenye umri wa kati ya miaka 16 na 19 katika maeneo ya mashambani wanaojiondoa shuleni ilishuka kwa asilimia 20 na watoto waliripotiwa kurefuka kwa nusu inchi.

Hofu za hapo awali kuwa mradi huo ungehimiza familia kubaki nyumbani na kungojea msaada badala ya kufanya kazi zilibainika kuwa hazina msingi. Badala yake, kumerekodiwa vijisababu vichache zaidi vinavyotokana na kutojali, kwa mfano, watoto sasa hawawezi kuenda kuombaomba mitaani badala ya kuenda shuleni kwa hofu ya kuwa wakifanya hivi, watatolewa katika mpango huu. Misaada kutoka kwa mashirika yasiyo ya kiserikali inaweza kuwa na ufanisi zaidi kuliko kiserikali unaweza kuwa bora zaidi kuliko ule wa serikali kwa kuwa mashirika haya yanawafikia maskini katika maeneo ya mashambani na yana usimamizi bora zaidi

Mojawapo kati ya njia zilizopendekezwa kusaidia nchi maskini ni ile ya msamaha wa madeni. Kutokana na hali ilivyo katika nchi nyingi ambazo hazijaendelea na zilizo na madeni makubwa ya benki na madeni ya serikali za nchi tajiri, na pia kutokana na riba ambayo zinapaswa kulipa kutokana na madeni haya (mara nyingi hupita kiwango cha fedha ambazo nchi hizi zinaweza kuzalisha kama faida kila mwaka kutokana na mauzo), kufutwa kwa madeni haya kwa kiasi fulani au kikamilifu kutawezesha mataifa haya “kujitoa shimoni”. Nchi maskini zikiacha kutumia pesa zao kulipa madeni haya, zitaweza kutumia pesa hizo kwa mambo muhimu zaidi yanayosaidia kupunguza umaskini kama vile kutoa huduma za kimsingi za afya na elimu. Mataifa mengi yalianza kutoa huduma, kama vile huduma za bure za afya kuanzia hapo awali ingawa miundombinu ya afya haingehimili hayo. Yaliweza kufanya hivi kutokana na akiba za awamu kadhaa za kusamehewa madeni mwaka 2005.

Mojawapo ya mbinu mpya zinazopendwa za kiteknolojia zinazohakikisha ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini ni mikopo midogo iliyoanzishwa na Benki ya Grameen mwaka wa 1976 nchini Bangladesh. Dhana hapa ni kuwapa wakulima au vijiji mikopo midogo ili waweze kununua vitu wanavyovihitaji ili kuogeza mapato yao. Mfano maalum ni ule wa Benki ya Watu ya serikali ya Uthai inayotoa mikopo ya kati ya Dola 100 na 300 kuwasaidia wakulima kununua vifaa au mbegu, kuwasaidia wauzaji wa mtaani kununua bidhaa za kuuza au kuwawezesha wengine kufungua maduka madogo. Pia, biashara ndogo ndogo katika Jamhuri ya Dominika ni kuwawezesha wanawake wengi kupata ajira na kulipwa mapato yao wenyewe. Wakati kuendeleza mwanamke na msimamo wake wa kaya kiuchumi, microloans kuwawezesha wanawake na kuwawezesha voice maoni yao katika kaya ujumla maamuzi.

Watu wengine wanasema ya kuwa kupokea misaada kutoka nchi za Ulaya kila mara huongeza umaskini na ukosefu wa usawa katika jamii kwa kuwa misaada hii huandamana na vikwazo vinavyoathiri vibaya uchumi wa nchi zinazopokea msaada, au kwa kuwa inaandamana na uagizaji wa bidhaa kutoka nchi wafadhili bila kuzingatia kuwa bidhaa hizo zingepatikana kwingineko kwa bei nafuu, au kwa kuwa msaada wa kigeni unaonekana kuwa unafaidi zaidi nchi wafadhili kuliko nchi inayopokea msaada. Wakosoaji pia wanasema ya kuwa sehemu ya msaada kutoka nchi za nje huibwa na serikali na maafisa wafisadi na kuwa kuongeza kiwango cha msaada kunaharibu ubora wa uongozi. Sera huelekezwa zaidi upande wa mbinu za kupata pesa zaidi za msaada kuliko kukidhi mahitaji ya wananchi. Wale wanaounga mkono msaada wanasema ya kuwa matatizo haya yanaweza kutatuliwa kwa kuweka mbinu bora za ukaguzi wa namna pesa hizi zinatumika. Kampeni za chanjo kwa watoto kama vile polio ugonjwa wa kuambukizwa wa koo na ugonjwa wa surua zimeokoa mamilioni ya watu.

Taasisi bora

Taasisi zinazoendeshwa vizuri bila ufisadi na zinazofuata sheria huunda na kuweka sheria zinazolinda usalama wa mali na biashara. Serikali za haki zinazoendeshwa vizuri zinapaswa kufanya uwekezaji katika miradi ya kitaifa inayochukua muda mrefu badala ya kupora mali kwa njia ya ufisadi. Wachunguzi katika Chuo Kikuu cha California Berkely waliunda walichokiita “Kipimo cha Weberianness” ambacho hupima vipengee mbalimbali vya urasimu na serikali ambavyo Max Weber alisema kuwa ni muhimu zaidi kwa serikali iliyoendeshwa kwa misingi ya fikira zinazokubalika na sheria zaidi ya miaka 100 iliyopita. Uchunguzi linganishi umeonyesha ya kuwa kipimo hiki kina uhusiano na vipimo vya juu vya maendeleo ya kiuchumi. Wakifuata dhana yao inayofuata mkondo sawa na huu ya uongozi bora, wachunguzi kutoka Benki ya Dunia wamepata matokeo yanayofanana: Takwimu kutoka nchi 150 imeonyesha kuwa viwango kadhaa vya kukadiria uongozi bora (kama vile uwajibikaji, ufanisi, utawala wa kisheria, kiwango cha chini cha ufisadi) vina uhusiano na viwango vya juu vya maendeleo ya kiuchumi. Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) ulichapisha ripoti mnamo Aprili 2000 kuhusu uongozi bora katika mataifa maskini kama njia kuu ya kuhakikisha maendeleo ya kiuchumi na kuushinda ubinafsi wa tabaka la matajiri ambao huwa na ushawishi mkubwa katika nchi hizo. Ripoti hiyo inamaliza kwa kusema ya kuwa “Bila ya utawala bora, mataifa haya yakiendelea kutegemea mtindo wa maendeleo ya kiuchumi yanayotokana na msaada kutoka juu na yanayotiririka mashinani na mbinu zingine, hayatafaulu.”

Mifano ya nchi zilizo na uongozi bora unaoleta maendeleo ya kiuchumi na kupunguza umaskini ni kama Thailand, Taiwan, Malaysia, Korea ya Kusini na Vietnam, ambazo kwa kawaida huwa na serikali thabiti. Nchi hizo zina nia na uwezo wa kuunda na kuweka sera zitakazoleta maendeleo ya muda mrefu yatakayowasaidia wananchi wote, si tu matajiri. Kampuni za kimataifa hudhibitiwa ili kuhakikisha ya kuwa zinafuata kanuni zinazofaa kuhusu malipo na ajira ya wafanyakazi, zinatozwa ushuru kwa kiwango kinachofaa ili kuleta maendeleo nchini na sehemu ya faida hubaki katika nchi hizo.Faida hii huwekezwa tena ili kusaidia katika maendeleo ya nchi. Katika mwaka wa 1975, nchi ya Korea Kusini ilikuwa na Pato la chini la Kitaifa kwa kila mtu ikilinganishwa na Ghana, na kufikia mwaka wa 2008, ilikua kwa kiwango cha mara 17 ya kile cha Ghana.

Fedha kutoka misaada na maliasili mara nyingi hugeuzwa na kuwekwa katika mikono ya watu binafsi na baadaye hupelekwa katika benki zilizo katika nchi za nje kutokana na ufisadi. Ikiwa benki za Ulaya zingekataa kuweka pesa zilizoibwa, kulingana na ripoti ya shirika la Global Witness, watu wa kawaida wangefaidika “kwa njia ambayo misaada ya kifedha haiwezi kufikia”. Ripoti hiyo ilipendekeza kuwekwa kwa sheria zinazoratibisha benki kwani hii inaweza kuwa njia bora ya kukatiza utumaji wa pesa za kigaidi, fedha chafu au kukosa kulipa ushuru.

Idadi ya watu

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Asilimia za wakazi wanaoishi kwa kiasi cha chini ya $ 1.25 kwa siku. Makadirio ya UN 2000-2006.
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Asilimia za wakazi wenye njaa, World Food Programme, 2006
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Matarajio ya kuishi.
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Human Development Index.
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Gini coefficient, kigezo cha tofauti za mapato, 2014.
Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Matarajio ya kuishi yameongezeka na kukaribiana duniani, isipokuwa Afrika Kusini kwa Sahara ambapo Ukimwi umerudisha nyuma. Jedwali linaonyesha miaka 1950-2005.


    Makala kuu: Ufukara nchi kwa nchi na Kizingiti cha ufukara

Umaskini uliokithiri

Umaskini hupimwa mara nyingi kama umaskini uliokithiri na umaskini wa kadri (cha mwisho kikiwa kipimo cha kutokuwa na usawa katika kiwango cha mapato). Umaskini uliokithiri unaashiria kipimo kilichowekwa ambacho hakibadiliki kamwe na ni sawa katika mataifa yote. Benki ya Dunia inafafanua umaskini uliokithiri kama kuishi kwa chini ya dola moja ya Marekani (uwezo wa ununuzi) kwa siku, na umaskini wa kadri kama kuishi kwa na chini ya dola mbili kwa siku. Inakadiria kuwa “mwaka 2001, watu bilioni 1.1 walikuwa na matumizi ya chini ya dola moja kwa siku na watu bilioni 2.7 walitumia chini ya dola mbili kwa siku.” Watoto milioni sita hufa kwa njaa kila mwaka-17,000 kila siku.

Idadi ya watu katika mataifa yanayoendelea wanaoishi katika umaskini uliokithiri ilishuka kutoka asilimia 28 mwaka 1990 hadi asilimia 21 mwaka 2001. Mengi ya maendeleo haya yametokea Mashariki na Kusini mwa Asia.

Kuhusu Asia Mashariki, Benki ya Dunia iliripoti kuwa “idadi ya watu walioishi kwa dola mbili kwa siku ilikadiriwa kushuka hadi asilimia 27 mwaka wa 2007, kutoka asilimia 29.5 mwaka wa 2006 na asilimia 69 mwaka wa 1990.”

Katika eneo la Afrika Kusini kwa Sahara umaskini uliokithiri ulipanda kutoka asilimia 41 mwaka 1981 hadi asilimia 46 mwaka 2001, ambao ukiungana na ongezeko la idadi ya watu, uliongeza idadi ya watu wanaoishi katika umaskini kutoka milioni 231 hadi milioni 318.

Mwanzoni mwa miaka ya 1990, baadhi ya nchi za Mashariki ya Ulaya na Asia ya Kati zilizokuwa na uchumi wa mpito, zilikabiliwa na kushuka kwa mapato kwa kiasi kikubwa.

Kuanguka kwa Umoja wa Kisovyeti kulisababisha kushuka kwa Pato la Kitaifa kwa kiwango kikubwa cha kati ya asilimia 30 na 35 kati ya mwaka wa 1990 na 1998 (ilipokuwa katika kiwango cha chini zaidi). Kutokana na hayo, viwango vya umaskini vilipanda, ingawa katika miaka ya baadaye, viwango vya mapato vilipoanza kupanda tena, viwango vya umaskini vilishuka kutoka asilimia 31.4 ya idadi ya watu hadi asilimia 19.6.

Takwimu za Benki ya Dunia zinaonyesha kuwa sehemu ya wananchi wanaoishi katika jamii zilizo na mapato yaliyo chini ya kiwango cha umaskini imeshuka katika kila eneo la dunia tangu mwaka 1990:

Eneo 1990 2002 2004
Asia ya Mashariki na Pacific 15.40% 12.33% 9.07%
Ulaya na Asia ya Kati 3.60% 1.28% 0.95%
Amerika Kusini na Caribbean 9.62% 9.08% 8.64%
Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika 2.08% 1.69% 1.47%
Asia Kusini 35.04% 33.44% 30.84%
Afrika Kusini kwa Sahara 46.07% 42.63% 41.09%

Ishara zingine za maendeleo pia zimekuwa zikiendelea kufanya vyema. Matarajio ya miaka ya kuishi pia yameongezeka kwa kiwango kikubwa katika nchi zinazoendelea tangu Vita vya Pili vya Dunia na yameanza kukaribia yale ya nchi zilizoendelea. Vifo vya watoto vimepungua katika maeneo yote yanayoendelea duniani.

Idadi ya watu duniani wanaoishi katika mataifa ambapo mgao wa chakula uko chini ya kalori 2,200 (Kilojuli 9200) kwa siku ilipungua kutoka asilimia 56 katikati ya miaka ya 1960 hadi chini ya asilimia 10 kufikia miaka ya 1990. Mienendo sawa na huo wa awali ilirekodiwa katika elimu, usambazaji wa maji safi na umeme na bidhaa za msingi zinazotumiwa na wanunuzi.

Vipimo hivi vimekosolewa na watu mbalimbali. Shaohua Chen na Martin Ravallion wanasema kuwa ingawa “ni wazi ya kuwa idadi ya watu fukara imeshuka... bila usawa katika maeneo yote... nchi zinazoendelea mbali na Uchina na India hazijafaulu kupunguza kwa kiwango cha maana idadi ya watu maskini. Kutokana na ongezeko la idadi ya watu duniani, idadi isiyobadilika ya watu maskini ingehusishwa na kiwango kinachopungua."

Tukitazama idadi ya wanaoishi kwa chini ya Dola moja kwa siku, bila kuhesabu Uchina na India, tunaona ya kuwa idadi hii ilipunguka kutoka asilimia 31.35 hadi 20.70 kati ya mwaka wa 1981 na 2004.

Ripoti ya 2007 ya Benki ya Dunia inayoitwa "Global Economic Prospects" inatabiri kuwa kufikia mwaka wa 2030, idadi ya watu watakaokuwa wakiishi kwa chini ya Dola moja kwa siku itakuwa imepungua kwa nusu, hadi watu milioni 550. Mwananchi wa kawaida anayeishi katika kile tulichokiita dunia ya tatu ataishi vyema sawa na namna ambavyo wananchi wa Ucheki na Slovakia wanavyoishi leo. Nchi nyingi za Afrika zitakuwa na matatizo ya kujaribu kufikia nchi nyingine zinazoendelea na hata ikiwa hali itabadilika kikamilifu, ripoti hii inaonya ya kuwa kufikia 2030, Afrika itakuwa na idadi kubwa zaidi ya watu maskini kuliko hali ilivyo sasa.

Sababu za ukuaji wa uchumi katika Mashariki mwa Asia na Asia ya Kusini zinatokana na kutoendelea kwao ikilinganishwa na maeneo mengine. Hii ni kulingana na nadharia ya kuja pamoja au nadharia ya sharti la kukusanyika pamoja. Kwa kuwa uchumi wa nchi hizi ulianza kupata usasa baada ya mataifa tajiri, uliweza kufaidika kwa kuiga maendeleo ya kiteknolojia yatakayouwezesha kuwa na viwango vikubwa zaidi vya uzalishaji ambavyo vimeundwa kwa karne nyingi katika mataifa tajiri.

Umaskini wa kadri

Umaskini wa kadri huangalia umaskini kama inavyoelezwa na jamii na unategemea muktadha wa kijamii, kwa hiyo umaskini wa kadri ni kiwango cha ukosefu wa usawa katika mapato. Kwa kawaida, umaskini wa kadri hupimwa kwa kuchukua idadi ya watu walio na mapato madogo zaidi ikilinganishwa na kiwango cha kawaida cha mapato. Kuna njia zingine tofauti za kupima ukosefu wa usawa wa mapato, kwa mfano Mgao wa Gini na Kipimo cha Theil.

Makadirio ya umaskini wa kadri hutumika kama viwango maalum vya kupima kiwango cha umaskini katika mataifa mengi yaliyoendelea. Takwimu hizi za umaskini hupima kutokuwa sawa badala ya ukosefu wa mali au shida. Vipimo hivi huwa vinafanywa kwa msingi wa mapato ya mtu binafsi ya kila mwaka na haviangalii ujumla wa mali. Kiwango cha umaskini kinachotumika katika mataifa wanachama wa OECD (Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo) na Muungano wa mataifa ya Ulaya ni yale yaliyo na misingi yake katika “umbali wa kiuchumi”, kiwango cha mapato kikiwa ni asilimia 60 ya mapato ya kadri ya kila nyumba.

Vipengee vingine

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Eneo la mabanda mjini Mumbai, India. Asilimia 60 ya wakazi wa Mumbai wapatao milioni 18 wanaishi katika maeneo ya mabanda.

Vipengee vya uchumi vya umaskini vinajihusisha na mahitaji ya kifedha, na hasa yale yanayohitajika katika maisha ya kila siku kama vile chakula, mavazi, nyumba, au maji salama. Umaskini, kwa mtazamo huu, unaweza kueleweka kama hali ambapo mtu au jamii inakosa mahitaji ya msingi inayohitaji ili kuishi vizuri na kuwa na maisha bora, hasa kutokana na ukosefu wa mapato unaoendelea.

Udadisi wa vipengee vya kijamii vya umaskini unaonyesha kuwa kuna uhusiano kati ya umaskini na ugawaji raslimali na mamlaka katika jamii na inaonyesha kuwa umaskini unaweza kuwa unatokana na upungufu wa “uwezo” wa watu kuishi maisha ambayo wangeyapendelea. Vipengee vya kijamii vya umaskini ni pamoja na ukosefu wa habari, elimu, huduma za afya]] au mamlaka ya kisiasa. Umaskini pia unaweza kueleweka kama kipengee kinacholeta tofauti za kitabaka katika jamii na ukosefu wa usawa katika uhusiano wa kijamii, unaojitokeza kwa njia ya kutengwa katika jamii, kuwategemea wengine na kupunguka kwa uwezo wa kujihusisha au kuendeleza uhusiano wa maana na watu wengine katika jamii.

Uchunguzi wa Benki ya Dunia wa “Sauti za Wanyonge”, ambao ilifanya uchunguzi kati ya watu maskini 20,000 katika mataifa 23, unaorodhesha mambo kadhaa ambayo watu maskini wametambua kuwa na uhusiano na umaskini. Hayo ni pamoja na:

  • Maisha ya kutojali
  • Maeneo yaliyotengwa
  • Vikwazo vya kimaumbile
  • Uhusiano kati ya wake na waume
  • Matatizo katika uhusiano wa kijamii
  • Ukosefu wa usalama
  • Utumiaji mbaya wa mamlaka
  • Kuondoa mamlaka katika taasisi
  • Uwezo uliowekewa vizuizi
  • Mashirika ya kijamii yasiyo na uwezo wa kutosha

David Moore, katika kitabu chake Benki ya Dunia, anasema ya kuwa udadisi mwingine wa umaskini unaonyesha dharau, na wakati mwingine ubaguzi wa rangi, na mtazamo mbaya kwa watu maskini unaowaonyesha kama watu wanyonge wanaongojea tu kupokea msaada.

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Camden, New Jersey ni moja ya majimbo maskini zaidi ya Marekani.

Ufukara uliokithiri, neno ambalo lilivumbuliwa na Michael Lipton, unaashiria hali ya kuhesabiwa kati ya watu maskini zaidi kati ya jamii maskini katika nchi zenye mapato madogo. Lipton alieleza ufukara uliokithiri kama kupokea chini ya asilimia 80 ya kiwango cha chini zaidi cha kalori kinachopaswa kuchukuliwa na mwili na wakati huo huo kutumia zaidi ya asilimia 80 ya mapato kununua chakula. Kwa upande mwingine, ripoti moja ya 2007 iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Uchunguzi kuhusu sera ya Chakula ilifafanua ufukara uliokithiri kama kuishi kwa chini ya senti 54 kwa siku. Shirika lisilo la kiserikali la BRAC limeanzisha mradi unaoitwa “Kuwalenga wanaoishi katika ufukara uliokithiri” unaonuia kutatua ufukara uliokithiri kwa kufanya kazi pamoja na wanawake fukara kwa kiwango binafsi.

Ufukara wa hiari

"'Tis the gift to be simple,
'tis the gift to be free,
'tis the gift to come down where you ought to be,
And when we find ourselves in the place just right,
It will be in the valley of love and delight."
—Shaker song.

Kati ya watu wengine, kama vile watawa, umaskini unachukuliwa kuwa jambo linalohitajika na kutamanika, na linapokewa kwa mikono miwili ili kuweza kufikia kiwango fulani cha kiroho, kitabia au kiakili.

Umaskini hueleweka kuwa kiungo muhimu cha kuachana na mambo ya dunia katika dini kama vile Ubuddha (kwa watawa pekee, si kwa wafuasi wengine) na wafuasi wa Ujaini, ilhali kwa Wakatoliki hii ni moja kati ya mashauri ya Kiinjili.

Mashirika kadhaa huwa na nadhiri ya kuishi katika hali ya ufukara. Kwa mfano itikadi za wafuasi wa Mtakatifu Fransisko wa Asizi zinapinga umiliki wowote wa mali katika ngazi ya mtu binafsi au katika jumuia.

Ingawa umiliki wa mali na bidhaa haukubaliwi kwa wafuasi wa Mtakatifu Benedikto wa Nursia, kufuatia kanuni ya Mt. Benedikto, monasteri zimekubaliwa kumiliki mali na pesa na historia inaonyesha kuwa makao kadhaa ya watawa hao yalikusanya mali nyingi mno.

Katika muktadha huo wa nadhiri za kitawa, umaskini unaeleweka kama njia ya kujinyima ili kuhudumia wengine. Mwaka wa 1217 Papa Honorius III aliandika kwamba wafuasi wa Mtakatifu Dominiko Guzman "waliishi maisha ya umaskini wa hiari, wakijitia hatarini na kuteseka, ili wengine wapate kuokolewa”.

Kufuatia tahadhari ya Yesu kuwa mali ni kama miiba ambayo huzuia mbegu nzuri ya Neno la Mungu kukua (Math 13:22) umaskini wa hiari unaeleweka na Wakristo kama jambo lenye faida kuu kwa mtu binafsi - njia ya kujiadilisha ambapo mtu hujitenga na vitu vingine vinavyovutia fikira zake na kumtenganisha na Mungu.

Mtazamo wa mifumo mbalimbali duniani

Mtazamo wa mifumo ya kidunia unatabiri ya kuwa mataifa yanayoendelea hayataweza kukua ipasavyo kiuchumi katika miaka ijayo ikiwa bado yana uwekezaji mkubwa wa makampuni ya kimataifa kutoka nchi zilizoendelea. Ingawa kuna tofauti kati ya mataifa hayo yanayoendelea, chunguzi kadhaa zilizofanywa na wanasosholojia zimeonyesha kuwa mengi ya mataifa yanayoendelea yaliyo na uwekezaji mkubwa kutoka mataifa yaliyoendelea yana ukuaji mdogo zaidi wa kiuchumi kwa muda mrefu. Hata hivyo, uchunguzi huo wote ulifanywa zaidi ya miaka ishirini iliyopita na ulitumia njia mbovu za kupata takwimu. Utafiti uliofanywa hivi karibuni unaonyesha kuwa kwa ujumla uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni hufaidi nchi pokezi ingawa athari zake si sawa kila mahali. Kutegemea sifa za nchi nyingine, huenda uwekezaji wa nchi za kigeni usiwe na athari yoyote, nzuri au mbaya, kwa maendeleo.

Nadharia za mfumo wa kidunia zinaonyesha ya kuwa sera bora zaidi inayoweza kufuatwa na nchi yoyote ni ile ya autarkia ama kufanya biashara na mataifa mengine yanayoendelea pekee. Hata hivyo, mataifa makubwa yaliyofuata sera hiyo kama vile Uchina na India kabla ya mwaka wa 1980 yalishuhudia kuzorota kwa uchumi na kuongezeka kwa umaskini. Baadhi ya mataifa ya Amerika ya Kusini ambayo pia yalijaribu kutegemea sera hiyo ya maendeleo kwa kutumia mtazamo wa ndani pia yalipata matokeo sawa na hayo. Inaonekana kuwa kuna sababu nyingi za athari mbaya ya utawala wa mataifa tajiri. Sababu kuu ni tatizo la kupotoka kwa miundo. Katika uchumi ambao haujapotoka maliasili huzindua mfululizo wa shughuli zinazoleta faida, nafasi za kazi na ukuaji. Tutachukua mfano wa nchi iliyoendelea na iliyo na idadi kubwa ya madini ya shaba ardhini. Nafasi za kazi zinapatikana na faida inatengenezwa kwanza kutokana na uchimbaji wa madini ya shaba. Kisha nafasi nyingine za kazi na faida zaidi inapatikana wakati shaba inapotengenezwa kuwa chuma na bidhaa hizi kuuzwa na kampuni ndogo ndogo, ,ambazo pia zinaongeza nafasi za kazi na faida. Kutokana na mchakato huu wote, kuna mfululizo wa nafasi za kazi na faida ambazo huleta ukuaji wa kiuchumi pamoja na mapato ambayo yanaweza kutumika kuendeleza nchi kwa ujenzi wa vitu kama barabara, umeme na taasisi za mafunzo. Lakini shaba ikichimbwa katika nchi inayoendelea na iliyo na uhusiano na nchi iliyoendelea, madini hayo yanapelekwa kwa nchi iliyoendelea ambako mfululizo wa kuitengeneza unamalizikia. Nafasi za kazi zilizosalia na faida zote zinzotokana na mfululizo wa shughuli hizi zinapotelea katika nchi zilizoendelea. Huu ni mfano wa kupotoka kwa miundo. Athari nyingine ni ile ya kuvurugwa kwa ukulima. Kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa kisasa wa dunia, ukulima ulikuwa unafanywa ili kukidhi mahitaji ya kijamii, na kulikuwa hakuna haja ya kutumia mbinu za kilimo za kupunguza kiwango cha ajira. Kutokana na mbinu hizi za awali na ukosefu wa soko kubwa kwa bidhaa, chakula kilikuwa kinauzwa kwa bei ya chini zaidi, sehemu ya mashamba iliachiwa wakulima wadogo, na nafasi za kazi zilikuwa nyingi zaidi. Hata hivyo, kutokana na ukulima wa mauzo katika nchi za nje na mbinu za kupunguza kiwango cha ajira kwa ukulima, chakula kimekuwa ghali zaidi, wakulima wadogo wanafukuzwa kutoka kwa mashamba ili nafasi zaidi ya kukuza bidhaa za kuuzwa katika soko la dunia ipatikane, na mashine zaidi zinatumiwa kufanya kazi, na hivyo kusababisha upungufu wa nafasi za kazi. Faida zinakiendea kikundi kidogo cha wanaomiliki ardhi na kampuni za kimataifa za kilimo, huku wasiomiliki ardhi wakipoteza kazi zao, ardhi, na mapato ambayo yananawazuia kuwa wanunuzi wanaohitajika kuhakikisha kukua kwa uchumi. Tatizo la tatu kwa mataifa yanayoendelea ni mizozano ya kitabaka. Tabaka la wenye uwezo wa kiuchumi na kisiasa katika mataifa yanayoendelea huwakaribisha zaidi watu kutoka tabaka la watu wanaomiliki makampuni kwa kuwa wanajua ya kwamba kampuni hizi zinafanya uwekezaji katika nchi zao kutokana na gharama ya chini ya ajira kiwango cha chini cha ushuru kutokuwa na vyama vya wafanyakazi, na mambo mengine kama vile sheria dhaifu za mazingara, ambazo zinajali zaidi masilahi ya makampuni hayo ya kimataifa.

Tazama pia

  • Nchi kulingana na kiwango cha kuzaa
  • Nchi kulingana na pato la taifa
  • Nchi kulingana na kiwango cha umaskini
  • Mzunguko wa umaskini
  • Kiwango cha maendeleo
  • Maradhi ya ufukara
  • Ugawaji wa mali
  • Usalama wa chakula
  • Njaa
  • Maendeleo ya kimataifa
  • Miaka anayotarajia mtu kuishi
  • Kiwango cha elimu
  • Ongezeko la idadi ya watu
  • Kitongoji duni
  • Watoto wa mitaani
  • Masilahi
  • Benki ya Dunia
  • Siku ya Chakula Duniani

Tanbihi

Kusoma zaidi

Viungo vya nje

Umaskini: Asili ya umaskini, Athari za umaskini, Kupunguza umaskini 
Wiki Commons ina media kuhusu:

Tags:

Umaskini Asili ya umaskiniUmaskini Athari za umaskiniUmaskini Kupunguza umaskiniUmaskini Idadi ya watuUmaskini Mtazamo wa mifumo mbalimbali dunianiUmaskini Tazama piaUmaskini TanbihiUmaskini Kusoma zaidiUmaskini Viungo vya njeUmaskiniAfyaBinadamuChakulaHudumaKiarabuMaji salamaMavaziNenoNyumbaUfukara

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Kitenzi kikuuMuda sanifu wa duniaUzazi wa mpango kwa njia asiliaJinsiaStadi za maishaFiston MayeleMkwawaBahatiKarafuuUchapajiSayariNyasa (ziwa)Uainishaji wa kisayansiSakramentiFigoNdimuKylian MbappéWaheheKiimboKinembe (anatomia)UbongoMapambano kati ya Israeli na PalestinaKanisa KatolikiMimba kuharibikaBikiraTaswira katika fasihiMuhammadMeno ya plastikiKombe la Dunia la FIFABaraKutoka (Biblia)Mnyoo-matumbo MkubwaVivumishi vya pekeeMaajabu ya duniaWanyamaporiTungo kiraiMkoa wa ShinyangaKupatwa kwa JuaMzabibuAbrahamuPesaOrodha ya Watakatifu wa AfrikaFasihiWairaqwKanuni ya Imani ya Nisea-KonstantinopoliAsili ya KiswahiliJokofuSimu za mikononiAbakuriaUtumwaAngahewaUandishi wa inshaWajitaPapaKipepeoOrodha ya Watakatifu WakristoUmoja wa UlayaUhakiki wa fasihi simuliziMajira ya baridiArsenal FCTetekuwangaMwenge wa UhuruMfumo wa JuaMfumo wa vyama vingiMpango wa BiasharaJérémy DokuNominoKishazi tegemeziMkoa wa MaraMbossoMahakama ya TanzaniaFalsafaNdovuMnazi (mti)Wayao (Tanzania)🡆 More