Senene

Senene (jina la kisayansi: Ruspolia differens ; jina la Kiganda: Nsenene; jina lililokosewa: panzi wenye pembe ndefu) ni mdudu wa familia Tettigoniidae katika oda Orthoptera.

Senene
Jika la Ruspolia nitidula anayefanana na senene
Jika la Ruspolia nitidula anayefanana na senene
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Orthoptera (Wadudu wenye mabawa manyofu)
Nusuoda: Ensifera (Wadudu kama senene)
Familia ya juu: Tettigoioidea
Familia: Tettigoniidae (Wadudu walio na mnasaba na senene)
Nusufamilia: Conocephalinae
Jenasi: Ruspolia
Schulthess, 1898
Spishi: R. differens
(Serville, 1838)

Wapo tele magharibi mwa Kenya na Tanzania, kusini mwa Uganda na kaskazini mwa Rwanda lakini anapatikana pia Afrika Kusini, Malawi, Cote d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ghana, Burundi, Kamerun, Zimbabwe, Zambia, Madagaska pamoja na Mauritius.

Baada ya majira ya mvua wapevu hukongomana katika makundi ya maelfu ya wadudu.

Spishi aina hii kwa muda mrefu imekuwa ikijulikana kama moja ya totems nyingi za Ufalme wa Buganda wa Uganda. Zilipatikana na Seruwu Douglass kutoka Visiwa vya Ssese huko Masaka.

Mara nyingi wadudu kama senene huitwa panzi, lakini senene wana vipapasio virefu sana kuliko pronoto na jike ana kiungo kama mfuo kinachofanana na kitara kinachotumika kwa kutaga mayai. Kinyume na hivyo panzi wana vipapasio vifupi na majike hawana kiungo kwa umbo la kitara.

Mara nyingi huchanganyikiwa na Ruspolia nitidula inayohusiana kwa karibu.

Kama chakula

Senene 
Senene tayari kwa kuliwa.

Wakati wapevu wa senene wakionekana watu huajili kuwakusanya ili kuwakaanga kama chakula. Nchini Uganda senene walikamatwa kwa desturi na wanawake na watoto. Baada ya kukaangwa chakula hiki kilitolewa kwa waume wa wanawake wale kwa malipo ya gomasi mpya (Kiganda: gauni ya kitamaduni). Ingawa wanawake walilazimishwa kufanya kazi hiyo ya kuchosha hawakuruhusiwa kula chakula hiki. Iliaminika kwamba wanawake wanaokula senene wangezaa watoto wenye kichwa cha umbo la kichwa cha senene. Siku hizi wanawake hula senene bila shida.

Nchini Tanzania chakula cha senene hupendwa sana na watu wa Bukoba, hasa kabila la Wahaya, na katikati na kusini-magharibi mwa Uganda, kikiwa pia chanzo muhimu cha mapato.

Marejeo

Tags:

Afrika KusiniBurundiCote d'IvoireFamilia (biolojia)GhanaJamhuri ya Kidemokrasia ya KongoJina la kisayansiKamerunKaskaziniKenyaKiganda (lugha)KusiniMadagaskaMagharibiMalawiMauritiusOdaOrthopteraPanziRwandaTanzaniaUgandaWaduduZambiaZimbabwe

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

TabainiMawasilianoFalsafaWamasaiTungoMisimu (lugha)Maneno sabaPichaJulian AssangeMweziBaruaSanaa za maoneshoMahakama ya TanzaniaTelevisheniAmfetaminiTaarabMaji ya chumviNyokaKiini cha atomuPasaka ya KikristoHali maadaNominoMkunduNyongoLongitudoBendera ya ZanzibarOrodha ya Watakatifu WakristoKima (mnyama)AsiaViwakilishi vya idadiWimbo wa TaifaOrodha ya Makamu wa Rais TanzaniaUsawa bahari wastaniMshororoAzimio la ArushaMtume PetroKarafuuProtiniMjusi-kafiriSiasaVita ya Maji MajiRayvannyBabaLugha ya kwanzaMaambukizi nyemeleziMwakaOsama bin LadenAsili ya KiswahiliNgeli za nominoKamusi elezoMkoa wa SimiyuWaswahiliHistoria ya Afrika KusiniFonimuAbedi Amani KarumeKadi za mialikoYouTubeSean CombsFIFARohoWagogoUmoja wa MataifaUtapiamloMazungumzoTabianchiBukayo SakaJuaPalestinaSenegalMuhammadArudhiMakaburuTamathali za semiKitabu cha ZaburiJumapili ya matawiMavaziDodoma (mji)Homa ya mafua🡆 More