Raga (ing.
Nje ya Jumuiya ya Madola mchezo huo ni maarufu Ufaransa, Argentina na Japani.
Rugby ilianzishwa nchini Uingereza sambamba na mpira wa miguu Wakati wa karne ya 19. American Football imezaliwa kutoka kwa rugby ya Kiingereza.
Shabaha ya mchezo ni kubeba au kukanyaga mpira kupitia timu ya wapinzani hadi goli na kuuingiza kwenye goli juu ya mti wa kulala.
Mpira una umbo la duaradufu. Timu mbili ambazo kwa kawaida huwa na wachezaji 15 zinashindana. Mpira unaweza kushikwa kwa mkono; kuna rukhsa kuupa kwa mchezaji mwingine au kuutupa nyuma. Lakini kuutupa mbele ni kosa ndogo unaofuatwa na tendo la "scrum". Hapo mpira unawekwa chini na wachezaji 8 wa kila timu wanashikamana na kusukumana hadi mchezaji mmoja anaweza kushika tena mpira.
Kuna rukhsa kumzuia mchezaji na kumwangusha kwa kumshika nyuma ya msari wa mabega. Tendo hili linaitwa "tackle". Akianguka china anapaswa kuachana na mpira. Wakati mchezaji analala chini wengine hawaruhusiwi kushika mpira kwa mikono.
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu. Je, unajua kitu zaidi kuhusu Raga kama historia yake, uenezi au kanuni zake? Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Raga, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.