Namba za Kiroma (kwa Kiingereza: Roman numerals) ni mfumo wa tarakimu kwa kuandika namba jinsi ulivyokuwa kawaida wakati wa Roma ya Kale na katika mwandiko wa Kilatini.
Mfumo huu unaendelea kutumika hadi leo kwa namba za pekee, hasa katika muundo wa orodha ambako mgawanyo ni wa ngazi mbalimbali. Ni kawaida kwa kutofautisha watu wenye jina lilelile, kwa mfano wafalme au mapapa: Malkia Elizabeth II (= wa pili) au Papa Benedikto XVI (= wa kumi na sita).
Jinsi ilivyo katika lugha mbalimbali, hata Waroma walitumia herufi za alfabeti ya Kilatini (ingawa chache) kama tarakimu za kutaja namba pia.
Herufi chache zilizotumika kwa namba muhimu zaidi, ambazo ziunganishwe kupata namba zote, ni:
I - 1
V - 5
X - 10
L - 50
C - 100
D - 500
M - 1000
Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba | Alama | Namba |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
I | 1 | V | 5 | X | 10 | L | 50 | C | 100 | D | 500 | M | 1000 |
Namba kubwa zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama inayotakiwa upande wa kulia lakini kwa kawaida si zaidi ya mara tatu:
I = 1; II = 2; III = 3, V ni 5 lakini VI ni 6; XX ni 20 lakini XXI ni 21.
Walikuwa na utaratibu wa kutoandika zaidi ya alama tatu ya aina ileile mfululizo. Lakini waliweza kupuuza utaratibu huu pia na kuandika VIIII (9) badala ya IX au XXXX (40) bafala ya XL.
Namba ndogo zaidi huonyeshwa kwa kuandika alama ndogo upande wa kushoto:
V ni 5 lakini IV ni 4 badala ya IIII (inayotokea mara chache); X ni 10 lakini IX ni tisa
Hapa walifuata utaratibu ufuatao: kuweka I moja au X moja au C moja tu kabla ya alama kuwba zaidi; halafu namba hii yatolewa kwenye namba kubwa:
I pekee huwekwa kabla ya V au X; X pekee kabla ya L au C; C pekee kabla ya D au M.
I | II | III | IV | V | VI | VII | VIII | IX | X |
1 | 2 | 3 | 4 | 5 | 6 | 7 | 8 | 9 | 10 |
XI | XII | XIII | XIV | XV | XVI | XVII | XVIII | XIX | XX |
11 | 12 | 13 | 14 | 15 | 16 | 17 | 18 | 19 | 20 |
XXI | XXII | XXIII | XXIV | XXV | XXVI | XXVII | XXVIII | XXIX | XXX |
21 | 22 | 23 | 24 | 25 | 26 | 27 | 28 | 29 | 30 |
XXXI | XXXII | XXXIII | XXXIV | XXXV | XXXVI | XXXVII | XXXVIII | XXXIX | XL |
31 | 32 | 33 | 34 | 35 | 36 | 37 | 38 | 39 | 40 |
XLI | XLII | XLIII | XLIV | XLV | XLVI | XLVII | XLVIII | XLIX | L |
41 | 42 | 43 | 44 | 45 | 46 | 47 | 48 | 49 | 50 |
LI | LII | LIII | LIV | LV | LVI | LVII | LVIII | LIX | LX |
51 | 52 | 53 | 54 | 55 | 56 | 57 | 58 | 59 | 60 |
LXI | LXII | LXIII | LXIV | LXV | LXVI | LXVII | LXVIII | LXIX | LXX |
61 | 62 | 63 | 64 | 65 | 66 | 67 | 68 | 69 | 70 |
LXXI | LXXII | LXXIII | LXXIV | LXXV | LXXVI | LXXVII | LXXVIII | LXXIX | LXXX |
71 | 72 | 73 | 74 | 75 | 76 | 77 | 78 | 79 | 80 |
LXXXI | LXXXII | LXXXIII | LXXXIV | LXXXV | LXXXVI | LXXXVII | LXXXVIII | LXXXIX | XC |
81 | 82 | 83 | 84 | 85 | 86 | 87 | 88 | 89 | 90 |
XCI | XCII | XCIII | XCIV | XCV | XCVI | XCVII | XCVIII | XCIX | C |
91 | 92 | 93 | 94 | 95 | 96 | 97 | 98 | 99 | 100 |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Namba za Kiroma, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.