Dwayne Michael Carter, Jr.
27 Septemba 1982) ni mshindi wa Tuzo za Grammy - akiwa kama rapa wa muziki wa hip hop bora kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Lil Wayne. Alijiunga na studio ya Cash Money Records akiwa bado yungali bwana mdogo na akabahatika kufanya rekodi kadhaa katika studio hiyo. Wayne alikuwa mmoja kati ya waliokuwa wanachama wa kikundi cha muziki wa rap cha Hot Boys.
Lil Wayne | |
---|---|
Lil Wayne mnamo 2011 | |
Maelezo ya awali | |
Amezaliwa | 27 Septemba 1982 |
Asili yake | New Orleans, Louisiana, United States |
Aina ya muziki | Hip hop |
Kazi yake | Rapa, Mwigizaji, CEO, Msanifu |
Ala | Sauti |
Miaka ya kazi | 1993–mpaka sasa |
Studio | Cash Money, Young Money, Universal |
Ame/Wameshirikiana na | Hot Boys, Birdman, T-Pain, Drake, Young Money, Kanye West, Young Jeezy, DJ Khaled, Mack Maine, Rick Ross |
Tovuti | www.lilwayne-online.com |
Alizaliwa kama Dwayne Michael Carter, Jr. na kukulia mjini Hollygrove karibu kidogo na mji wa New Orleans, Louisiana. Akiwa na umri wa miaka kumi na moja, akakutana na Bryan Williams, rapa na ndiyo mmiliki wa studio ya Cash Money Records. Baada ya makutano hayo, Wayne akarekodi rap flani ya michano katika studio hiyo ya Williams kwa kutumia chombo maalum cha kuweza kukujibu wakati unachana. Na kwa bahati nzuri michano hiyo ilimwacha hoi mmiliki huyo wa studio na kuthubutu hata kumwingiza Wayne katika studio yake. Wayne pia ana mtoto wa kike mmoja aitwaye Reginae Carter, aliyezaa na Bi. Antonia "Toya" Johnson, demu wake wa kitambo toka shule. Wawili hao walikuja kuoana wakati ule wa Siku Kuu ya Wapendanao ya mwaka wa 2004, lakini wawili hao walikuja kutarikiana mnamo mwaka wa 2006.
And
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Lil Wayne, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.