Abdul Juma Idd (maarufu kwa jina lake la kisanii Lava Lava; amezaliwa 27 Machi 1993) ni mwimbaji anayetokea Tanzania aliyesajiliwa chini ya lebo ya muziki WCB Wasafi inayomiliki wasanii wengine kama Rayvanny, Queen Darleen,Zuchu,Mbosso na Diamond Platnumz ambaye ndiye bosi wa lebo hiyo.
Lava Lava | |
---|---|
Taarifa za awali | |
Jina la kuzaliwa | Abdul Juma Idd |
Amezaliwa | Machi 27, 1993 (umri 30 ) |
Kazi yake |
Lavalava ni miongoni mwa vijana wanaofanya vyema kwenye muziki wa Bongo Fleva kwa sasa. Alijiunga WCB mwaka 2015 lakini alijulikana rasmi 22 Mei 2017.
Safari yake ya muziki ilianzia mtaani kwao, Bunju, Dar es Salaam ambapo alijenga jina lake kwa kuimba nyimbo za watu kiasi kwamba asipokuwepo mtaani hapo pengo lake huonekana.
Lavalava alitoroka shule na kwenda Tanzania House of Talents (kifupi: THT) kwa ajili ya kuimba, baada ya kupita kwenye mchujo wa wasanii wachanga zaidi ya 1000 na kuingia 50 bora, alifanya mafunzo ya muziki kwa miaka mitano na kukabidhiwa cheti cha masuala ya muziki na kupewa ruhusa ya kuingia mtaani kusaka au kutafuta menejimenti.
Baada ya kumaliza masomo yake aliomba nafasi WCB Wasafi na kubahatika kusajiliwa.
Albamu
Nyimbo
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Lava Lava (mwimbaji) kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Lava Lava (mwimbaji), which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.