L ni herufi ya 12 katika alfabeti ya Kilatini ambayo ni pia mwandiko wa Kiswahili cha kisasa.
Alfabeti ya Kilatini (kwa matumizi ya Kiswahili) | ||||||
---|---|---|---|---|---|---|
Aa | Bb | Cc | ch | Dd | ||
Ee | Ff | Gg | Hh | Ii | Jj | |
Kk | Ll | Mm | Nn | Oo | Pp | |
Rr | Ss | Tt | Uu | Vv | ||
Ww | Xx | Yy | Zz |
Asili yake ni Lambda ya alfabeti ya Kigiriki.
Kisemiti asilia Fimbo la kuchungia ng'ombe | Kifinisia Lamed | Kigiriki Lambda | Kietruski L | Kilatini L |
---|---|---|---|---|
Asili ya alama ni picha andishi iliyoonyesha fimbo la kuchungia ng'ombe. Wafinisia walirahisihsa alama hiyo na kuiita kwa neno lao la fimbo hili "lamed". Wakaitumia kama alama ya sauti "l". Wagiriki wa Kale wakaipokea kama "Lambda" na kubadilisha umbo lake kuwa kama paa ya nyumba.
Waetruski walipendelea umbo la kifinisia kwa kuiandika kama alama ya sauti "l". Waroma wa Kale wakageuza alama na kunyosha mikono yake kuwa L jinsi iliovyo hadi leo.
Makala hii kuhusu mambo ya elimu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu L kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article L, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.