Elizabeth II alikuwa malkia wa Ufalme wa Muungano wa Britania (Uingereza na Welisi na Uskoti) na Ireland Kaskazini tangu mwaka 1952 hadi kufariki dunia tarehe 8 Septemba 2022.
Alikuwa malkia kwa miaka 70 na siku 214. Katika historia yote ya dunia wako watawala wachache waliodumu madarakani muda mrefu kuliko yeye. Soma zaidi wasifu wake hapa Anafuatwa na mwana wake wa kwanza, Charles III wa Uingereza.
| |
Tarehe ya kuzaliwa | 21 Aprili 1926 |
Mahali pa kuzaliwa | Mayfair, Uingereza Ufalme wa Muungano |
Tarehe ya kifo | 8 Septemba 2022 (umri 96) |
Alizaliwa kwa jina la Elizabeth Alexandra Mary Windsor mjini London tarehe 21 Aprili 1926 kama mtoto wa kwanza wa mfalme George VI wa Uingereza na Elizabeth Bowes-Lyon.
Alitangazwa kuwa malkia tarehe 6 Februari 1952 mara moja baada ya kifo cha baba yake George VI. Wakati ule alikuwa akitembelea Kenya iliyokuwa bado koloni la Uingereza akatembelea milima ya Aberdare.
Alipokea taji katika ibada rasmi tarehe 2 Juni 1953 kwenye kanisa la Westminster Abbey.
Kama mkuu wa Jumuiya ya Madola alikuwa pia mkuu wa dola wa nchi zifuatazo ndani ya jumuiya hii:
Katika nchi zote aliposhika cheo hakuwa na mamlaka ya kiserikali ila alitawala kama mfalme wa kikatiba katika muundo wa serikali ya kibunge.
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Elizabeth II wa Uingereza kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Elizabeth II wa Uingereza, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.