Bulawayo ni mji mkubwa wa pili wa Zimbabwe wenye wakazi 665,940 (sensa ya 2022).
Iko kusini-magharibi ya nchi hiyo, katikati ya Matabeleland. Wakazi walio wengi ni Wandebele.
Jina la mji linatokana na neno la Kindebele "Kwabulawayo" yaani "machinjoni".
Mji wa leo ulijengwa juu ya mabaki ya boma la mfalme Lobengula. Lobengula aliwahi kujenga boma lake la kwanza 1871 takriban kilomita 15 kusini ya mji. Mwaka 1881 alihamia penye mji wa sasa.
Mwaka 1893 ufalme wa Lobengula ulishambuliwa na jeshi la Cecil Rhodes na mfalme aliamua kuchoma boma lake alipoona alishindwa kuzuia maadui. Waingereza walianzisha mji wao juu ya mabaki ya makazi ya awali. 1897 ilipewa cheo cha manisipaa na kuungwa na reli.
Bulawayo ilikuwa mji ambako upinzani dhidi ya ukoloni ulianza na baadaye kitovu cha upinzani dhidi ya serikali ya Robert Mugabe.
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Bulawayo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Bulawayo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.