Ali Ibn Abu Talib (Kar.: علي ابن أبي طالب * mnamo 600 BK Makka - + Januari 661 Kufah / Irak) alikuwa mkwe wa mtume Muhammad, khalifa wa nne wa Uislamu na imamu wa Shia wa kwanza.
Alikuwa pia baba wa wajukuu wa pekee wa mtume.
Aheshimiwa na Washia kama mfuasi wa kweli wa pekee wa mtume.
Ali alikuwa binamu wa Mohammed na kati ya wafuasi wa kwanza wa mtume. Alimwoa Fatimah binti wa mtume akazaa naye watoto watano: * Hasan ibn Ali (imamu wa pili wa Shia)
Baada ya kifo cha Muhammad mwaka 632 swali la kiongozi mpya wa umma wa Waislamu likaleta fitina kati ya wafuasi wa Ali na wengine iliyosababisha hadi leo mgawanyo kati ya Wasunni na Washia.
Mkutano wa viongozi Waislamu ulimchagua Abu Bakr kuwa khalifa wa kwanza badala ya Ali aliyedai ya kwamba aliteuliwa na mtume mwenyewe kuwa kiongozi baada yake. Hata baada ya kifo cha Abu Bakr wakateuliwa mara mbili makhalifa wengine yaani Umar ibn al-Khattab kama khalifa wa pili halafu Uthman ibn Affan kama khalifa wa tatu.
Ni baada ya kuuawa kwa Uthman tu ya kwamba Ali alichaguliwa khalifa wa nne. Alihamia Kufa nchini Irak penye kituo kikubwa cha jeshi la Uislamu.
Tangu mwanzo aliona upinzani wa vikundi mbalimbali si Waislamu wote waliomkubali:
Tar. 22 Januari 661 Ali aliuawa na Mkharijiya huko Kufa. Watoto wake Hasan na Husain walishindwa kumfuata kwa sababu Muawiya alichukua utawala akiwa khalifa wa tano.
Swali hili la uongozi ulisababisha fitina na mgawanyo kati ya Waislamu. "Shiat Ali" (chama cha Ali) ilikuwa sasa mwendo wa pekee ndani ya Uislamu uliodai ya kwamba uongozi wapaswa kuwa mkononi wa familia ya mtume hivyo wa watoto na wajukuu wa Ali na Fatimah.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ali ibn Abu Talib, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.