Fedha kwa maana ya malipo au sarafu angalia makala ya pesa
Fedha (kutoka Kiarabu فضة fiddtan) ni elementi na metali yenye kifupi cha Ag (kutoka Kilatini: argentum) na namba atomia 47 katika mfumo radidia. Uzani atomia ni 107.86. Fedha huyeyuka kwa 1234.93 K (961.78°C) na kuchemka kwa 2435 K (2162°C).
Kiasili yatokea kama metali nyeupenyeupe na laini au kama mchanganyiko katika madini. Kati ya metali zote fedha ni wayaikaji na inapitisha vizuri umeme.
Huhesabiwa kati ya metali adimu na katika historia imetumiwa mara nyingi kama metali ya kutengenezea sarafu. Kwa sababu hiyo mara nyingi kwa Kiswahili neno "fedha" linatumiwa sawa na "pesa" au "sarafu".
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Fedha kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Fedha, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.