Mauritania ni nchi ya Afrika kaskazini-magharibi.
Upande wa magharibi kuna pwani ya bahari ya Atlantiki, upande wa kusini imepakana na Senegal, upande wa mashariki na Mali na Algeria, upande wa kaskazini na Sahara ya Magharibi inayotawaliwa na Moroko.
Mauritania |
---|
Jina limeteuliwa kutokana na Mauritania ya kale iliyokuwa ufalme wa Waberber kusini kwa Mediteranea katika eneo la Algeria na Moroko ya leo.
Mji mkuu ni Nouakchott. Mji wa pili na kitovu cha uchumi ni bandari ya Nouadhibou karibu na mpaka wa Sahara Magharibi.
Mauritania ina wilaya 12 (zinaitwa "wilāyah").
|
Mnamo Machi 2007 wananchi walipata nafasi ya kumchagua rais mara ya kwanza katika historia ya nchi tangu uhuru. Sidi Ould Cheikh Abdallahi alishinda katika duru ya pili kwa 53% za kura zote akaapishwa tarehe 20 Aprili 2007.
Wakazi wengi (70%) ni Wamori, mchanganyiko wa Waarabu, Waberber na Waafrika waliotokana na watumwa kutoka kusini kwa Sahara. Asilimia 30 zilizobaki ni makabila ya Kiafrika yasiyoongea Kiarabu, ambacho ndicho lugha rasmi.
Upande wa dini, karibu wote ni Waislamu (hasa Wasuni). Uhuru wa dini unabanwa sana kwa nyingine zote.
Pamoja na hayo, hadi leo asilimia 4 za wakazi ni watumwa, ingawa mwaka 2007 ilifutwa haki ya kuwamiliki.
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mauritania kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mauritania, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.