Kuhusu matumizi ya jina Zohali kwa sayari hii tazama kipengele cha "Asili ya jina"
Uranusi | |
---|---|
Picha yenye rangi halisi ya Uranusi kama ilivyoonwa na Voyager 2 mnamo 22 Januari 1986. | |
Ugunduzi | |
Mgunduzi | William Herschel |
Tarehe | 13 Machi 1781 |
Jina | |
Asili ya jina | Kla. Ūranus, kutokana na Kgk. Οὐρᾰνός (Ouranós) |
Alama | |
Tabia za njiamzingo | |
Umbali mfupi | km 2,735,560,000au 18.2861 |
Umbali mrefu | km 3,006,390,000au 20.0965 |
km 2,870,972,000au 19.19126 | |
Uduaradufu | 0.04717 |
siku 30,688.5miaka 84.0205 | |
Mwinamo | 0.773° toka njia ya Jua |
Miezi | 27 |
Tabia za kimaumbile | |
km 25,362±7mara 3.976 ya Dunia | |
Tungamo | kg 8.6810×1025mara 14.536 ya Dunia |
g/cm3 1.27 | |
Uvutano wa usoni | m/s2 8.69 |
Kasi ya kuponyokea | km/s 21.3 |
siku −0.71832 | |
siku −0.71833 | |
Weupe | 0.300 (Bond)0.488 (jiometri) |
Halijoto | K 76 (−197.2°C) |
Uranusi ni sayari ya saba kutoka Jua.
Waswahili wa kale hawakujua sayari hii. Uranusi ni jina la kimataifa lililoteuliwa katika karne ya 19 baada ya majadiliano marefu kati ya wanaastronomia wa Ulaya. Ni jina la mungu wa Ugiriki ya Kale Urano (Kgi.Οὐρανός) aliyeaminiwa kuwa mungu wa anga. Lugha nyingi duniani zimepokea jina hili kwa sababu astronomia ya zamani haikujua sayari hii.
Vitabu kadhaa vinatumia jina la Kiswahili Zohali kwa kufuata kamusi ya KAST; lakini hili ni jina la Kiswahili kwa sayari ya sita (Kng. Saturn).
Ni sayari kubwa ya tatu ya Mfumo wa Jua hata kama mada yake ni hasa gesi iliyoganda. Jumla ya masi yake ni mara 14 ya dunia hivyo ni sayari nyepesi kulingana na ukubwa wake. Kipenyo chake ni takriban kilomita 50,000.
Inazunguka Jua kwenye obiti inayochukua miaka 84. Umbali wake na Jua ni takriban mara 19 umbali wa Jua na Dunia au kilomita bilioni 2.9; afeli yake ni vizio astronomia 20.11 na periheli yake ni vizio astronomia 18.33.
Hadi mwaka 2023 miezi 27 iligunduliwa. Miezi mikubwa huitwa Miranda, Arieli, Umbrieli, Titania na Oberoni. Ina pia pete kadhaa yaani mawingu ya vumbi, barafu na mawe madogo ambayo ni nyembamba na kuzunguka sayari kwa umbo la pete. Pete za Uranusi ni hafifu kuliko zile za Zohali.
Uranusi inaonekana kama nyota hafifu sana yenye mwangaza wa 5.6 - 6. Kutokana na kuwa hafifu vile na mwendo wake wa pole hakuna utamaduni wowote wa kale ulioitambua kuwa sayari. Ilitambuliwa mara ya kwanza kuwa sayari na tarehe 13 Machi 1781 na William Herschel.
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Uranusi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uranusi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.