Eire (pia: Ireland, Ayalandi; kwa Kiingereza mara nyingi Republic of Ireland) ni nchi ya kisiwani katika funguvisiwa la Britania ya Ulaya.
Eire |
---|
Eire ilitawaliwa na Uingereza hadi mwaka 1922. Sehemu ya kaskazini ya kisiwa imebaki kama sehemu ya Ufalme wa Muungano (pamoja na Uingereza, Uskoti na Welisi).
Mji mkuu ni Dublin.
Kijiografia Eire ni kisiwa kilichogawiwa kati ya Jamhuri ya Eire inayokalia sehemu kubwa ya kisiwa na Northern Ireland ambayo ni jimbo la Ufalme wa Maungano. Kisiwa chote kina eneo la km² 84,421 na 83% zake ni Jamhuri ya Eire.
Upande wa magharibi kuna Bahari ya Atlantiki, upande wa mashariki Bahari ya Eire inayokitenga na kisiwa cha Britannia.
Kitovu cha kisiwa kuna tambarare inayozungukwa nje upande wa pwani na vilima.
Mlima mrefu zaidi ni Carrauntoohil wenye kimo cha mita 1,038.
Mto mkubwa ni Shannon ambao kutoka kaskazini unaelekea kusini. Kwenye tambarare ya katikati kuna maziwa kadhaa.
Hali ya hewa inaathiriwa na Atlantiki: ni ya wastani, hakuna baridi kali wala joto kali.
Bahari inaleta mvua nyingi na hivyo Eire huitwa "Kisiwa cha Kijani".
Miji mikubwa ni Dublin (wakazi milioni 1), Cork (watu 190,000), Limerick (90,000), Galway (72,000) na Waterford (49,000).
Kwa karne kadhaa Eire ilitawaliwa na Uingereza.
Sheria ya mwaka 1800 iliunganisha Ufalme wa Britania Kuu na Ufalme wa Eire na hivyo kuunda Ufalme wa Muungano (United Kingdom of Great Britan and Ireland).
Baada ya Vita vya uhuru vya Eire bunge la London kwa sheria ya mwaka 1920 (Government of Ireland Act 1920) liligawa Ireland katika sehemu mbili za Northern Ireland na Southern Ireland.
Wabunge waliochaguliwa katika Ireland ya Kusini walijitangaza kuwa bunge la Eire na kwa mapatano ya mwaka 1922 uhuru wa Eire ulitambuliwa. Nchi mpya ilijiita tangu 1937 "Jamhuri ya Eire" na kuendelea kama nchi ya pekee.
Baada ya uhuru wa sehemu kubwa ya kisiwa hicho, ile ya kaskazini-mashariki imebaki kama sehemu ya Ufalme wa Muungano.
Wakazi walio wengi (82.2%) ni Waeire asili, Wazungu wengine ni 9.5%, Waasia 2.1%, Waafrika 1.2% n.k.
Wengi hutumia lugha ya Kiingereza lakini lugha ya Kieire ni lugha ya kwanza ya taifa. Kinazungumzwa katika maeneo kadhaa ya vijijini na hufundishwa shuleni, lakini kutokana na uhamiaji, Kipolandi kina wasemaji wengi zaidi.
Upande wa dini, 78.3% ni Wakatoliki na 4.2% ni Wakristo wa madhehebuya Uprotestanti na 1.3% ni Waorthodoksi. Ushiriki wa ibada ni wa juu sana. Waislamu ni 1.3% na 9.8% hawana dini.
Nchi za Umoja wa Ulaya | |
---|---|
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi |
Makala hii kuhusu maeneo ya Ireland bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Eire kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Eire, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.