Uswisi ni nchi ya Ulaya isiyo na pwani katika bahari yoyote.
Uswisi |
---|
Imepakana na Ujerumani, Ufaransa, Italia, Austria na Liechtenstein.
Jina rasmi ni Confoederatio Helvetica (kwa Kilatini: Shirikisho la Kiswisi).
Majimbo yake 26, ambayo huitwa "kantoni", yanajitawala.
Shirikisho la Uswisi lilianza mwaka 1300 hivi kutokana na ushindi vitani dhidi ya Austria na Burgundy.
Uhuru wa shirikisho kutoka Dola Takatifu la Kiroma ulitambuliwa rasmi katika Amani ya Westphalia mwaka 1648.
Uswisi imepata umaarufu hasa kutokana na sababu zifuatazo:
Mji mkuu wa shirikisho ni Bern.
Mji mkubwa ni Zürich wenye benki nyingi.
Mji wa Geneva ni kati ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa; ni pia makao makuu ya kimataifa ya Umoja wa shirika za Msalaba Mwekundu na mashirikia mengine ya kimataifa.
Hata hivyo Uswisi imekuwa kati ya nchi za mwisho kujiunga na UM (2002).
Kuna lugha rasmi 4: Kijerumani (62.8%), Kifaransa (22.9%), Kiitalia (8.2%) na Kirumanj (0.5%). Lakini wengi wanajua na kutumia lugha zaidi ya moja.
Kati ya lugha za kigeni zinazotumika nyumbani, zinaongoza Kiingereza (5%), Kireno (3.8%), Kialbania (3%), Kihispania (2.6%), Kiserbokroatia (2.5%) n.k.
Upande wa dini, kati ya wakazi, 68% ni Wakristo, hasa Wakatoliki (37.2%) na Wakalvini (25%), lakini pia Waorthodoksi (2.3%) na wengineo. 5.1% ni Waislamu (hasa wahamiaji). 24% hawana dini maalumu.
Makala hii kuhusu maeneo ya Uswisi bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Uswisi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uswisi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.